• HABARI MPYA

    Monday, August 06, 2012

    WABUNGE WAPITISHA SERA YA KUICHANGIA YANGA MAMILIONI KILA MWAKA

    Mh Misanga akitambulisha Tawi la Yanga Bungeni, kulia kwake ni Manji, Martha na Mkuchika na kushoto na Mama Karume na Kifukwe

     Na Mahmoud Zubeiry
    WABUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, ambao ni wapenzi wa Yanga watakuwa wakichangia Sh. 500,000 kila mwaka katika kuchangia maendeleo ya klabu hiyo, hayo yamefikiwa leo katika ukumbi mdogo wa Bunge mjini Dodoma, wakati wa hafla ya fupi ya uzinduzi wa Tawi la Yanga Bungeni.
    Hiyo ilifuatia ombi la Mjumbe wa Baraza la Wadhamini la klabu ya Yanga, Mama Fatuma Karume, mke wa rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amaan Karume leo wakati akizindua tawi la Yanga Bungeni.
    Mama Karume alizindua mfuko huo kwanza yeye mwenyewe kutoa Sh. 500, 000 ambazo zilipokewa na Mweka Hazina wa Tawi la Yanga Bungeni, Martha Moses Mlala, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Singida.
    Wabunge wengine waliotoa fedha zao hapo hapo ni Abbas Mtemvu (Temeke, CCM). Athumani Mfutakamba (Igalula, CCM) na Grace Kiwelu (Viti Maalum, CCM).
    Awali, akisoma taarifa ya tawi hilo, Mwenyekiti Misanga ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Yanga miaka ya 1970, chini ya Mwenyekiti Juma Shamte, alisema kwamba Julai 31 walifanya uchaguzi wa viongozi wa tawi la klabu hiyo Bungeni na mbali ya yeye kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti, Abadallah Ameir alichaguliwa kuwa Makamu wake.
    Alisema Nafasi ya Katibu Mkuu, ilikwenda kwa Godfrey Zambi, Katibu Msaidizi, Grace Kiwelu, Mweka Hazina Martha Mlala na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Abbas Mtemvu, Halima Mdee, Victor Mwambalaswa, Mohammed Chambo, Abdul Marombwa, Vicky Kamatta na Ritta Kabati.
    Aidha, alisema waliteua pia Kamati ya Ushauri ya Wajumbe wanne, ambao ni George Mkuchika, Zarina Madabida, Faki Makame na Chirtopher Chiza.  
    Pamoja na hayo, Misanga aliupongeza uongozi mpya wa Yanga chini ya Mwenyekiti wake Manji, na kuutaka uwe makini na wanachama wapandikiza sumu za migogoro klabuni.
    Tawi hilo jipya la Yanga, limepanga kuwafuturisha wachezaji wa Yanga jioni ya leo, kabla ya kurejea Dar es Salaam. 

    Mh Mkuchika na Manji

    Martha akihesabu michango ya Wabunge wenzake

    Mh Zambi kulia akifungua kikao 

    MAKOCHA; Kutoka kulia ni Tom, Minziro na Samatta

    Waheshimiwa Yanga damu

    Tegete na Chuji

    WALIOTOKEA SIMBA KIVYAO; Kutoka kulia Gumbo, Barthez na Yondan

    Mh Mtemvu, akizungumza na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe katika utambulisho wa Tawi la Yanga Bungeni

    Meza kuu

    Manji na Misanga

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WABUNGE WAPITISHA SERA YA KUICHANGIA YANGA MAMILIONI KILA MWAKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top