Bolton itampa ofa ya kuendelea kubaki klabuni Fabrice Muamba katika nafasi nyingine, baada ya kiungo huyo kulazimika kustaafu soka, miezi mitano baada ya kupoteza fahamu uwanjani kwa tatizo la moyo.
Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya Muamba kuonana na mtaalamu bingwa wa matatizo ya moyo, Pedro Brugada nchini Ubelgiji wiki iliyopita. Pamoja na hayo, upasiaji wa kusafisha moyo wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ulikwenda vizuri.
Bolton's Fabrice Muamba alipata mataizo ya moyo Machi, mwaka huu
Muamba (katikati) akiwa na famili ya klabu katika siku ya kufurahia, Jumapili
Muamba akiwa amebeba Mwenge wa Olimpiki Waltham Forest
Muamba alipata matatizo ya moyo Uwanja wa White Hart Lane mwezi Machi
Wachezaji wa Bolton na Spurs na kocha wa Wanderers, Owen Coyle (katikati),wakimuangali Muamba akipatiwa huduma ya kwanza
Meseji kibao za kumtakia kupona haraka Muamba zikiwa zimewekwa katika Uwanja wa Bolton, Uwanja wa Reebok, wakati alipokuwa hospitali
Dunia ya soka iliungana kumtumia ujumbe wa kumuombea kupona mapemaMuamba
Muamba na mtaalamu wa moyo, Dk Andrew Deaner (kushoto) na Mshauri wa masuala ya moyo, Dk Sam Mohiddin, madaktari ambao waliokoa maisha yake
Muamba akitoa machozi aliporejea kwenye Uwanja wa Reebok, Mei mwaka huu
Muamba akifuta machozi Uwanja wa Reebok, Mei mwaka huu
Muamba na mpenzi wake Shauna baada ya kupona
Muamba alipewa Shahada ya heshima Chuo Kikuu cha Bolton
Fabrice Muamba: Kutoka Kinshasa hadi Ligi Kuu England
1988: Alizaliwa April 6 mjini Kinshasa, Zaire (sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo).
1999: Alikwenda England akiwa ana umri wa miaka 11, kuungana tena na baba yake ambaye alikimbia vita Kongo.
2002: Alijiunga na timu ya vijana iliyoundwa na Arsenal - klabu ambayo alikuwa anaishabikia alipokuwa mdogo nyumbani kwao - kabla ya kuhitimu katika Akademi hiyo miaka miwili baadaye.
2005: Alisaini mkataba na Arsenal na kucheza mechi mbili za kikosi cha kwanza zote zikiwa za Kombe la Ligi dhidi ya Sunderland, Oktoba 25.
2006: Agosti alijiunga na Birmingham kwa mkopo wa muda mrefu na huko alicheza mechi 36 kabla ya kushinda tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa msimu.
2007: Me 11 - Alihamishiwa moja kwa Birmingham baada ya klabu hiyo kukubali kulipa pauni Milioni 4 Arsenal.
Agosti 21 - baada ya kuchezea timu zote za vijana za England kuanzia U-16s, Muamba alichezeshwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha England U-21 dhidi ya Romania, mechi ya kirafiki.
2008: Juni - Scores alifunga mabao mawili katika mechi 37 za ligi msimu wa 2007/08, lakini hakuinusuru Birmingham kushuka.
Agosti 7 - Alisaini Bolton baada ya Trotters kukubaliana dau la pauni Milioni 5 na Birmingham kwa ajili ya kiungo huyo.
2010: Agosti 10 - Alisaini mkataba mpya wa miaka minne Bolton, ambao ungemalizika mwaka 2014.
2011: Juni - aliichezea England U-21 katika michuano ya Mataifa ya Ulaya nchini Denmark.
Agosti 13 - alifunga bao lake la tatu katika ligi akiwa na Bolton ikiifunga 4-0 QPR.
Agosti 13 - alifunga bao lake la tatu katika ligi akiwa na Bolton ikiifunga 4-0 QPR.
2012: Machi 17 - Muamba alizimia uwanjani dakika ya 41, Bolton ikicheza mechi ya Kombe la FA naTottenham Uwanja wa White Hart Line, kabla ya kupelekwa katika hospitali ya London Chest, ambako alitibiwa hadi kupona.
Agosti 15 - Anatangaza rasmi kustaafu soka, baada ya kushauriwa na daktari.
Read more: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2188874/Fabrice-Muamba-career-Bolton-offer-job.html#ixzz23gQJIWog
0 comments:
Post a Comment