![]() |
| Kocha Kim kushoto akizungumza. Kulia Katibu wa TFF, Angetile |
Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa
Stars, Kim Poulsen amewaacha katika kikosi chake kinachoondoka alfajiri ya
kesho kwenda Botswana katika mchezo dhidi ya wenyeji Jumatano, wachezaji
wawili, kipa Deo Munishi ‘Dida’ na beki Shomary Kapombe kwa sababu ni majeruhi.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY usiku huu kwenye kambi
ya timu hiyo, hoteli ya Somaiya eneo la Gerezani, Dar es Salaam, kocha Kim
alisema anasikitika hatakuwa nao wachezaji hao kwenye safari kwa sababu ya
majeruhi.
Lakini Poulsen alisema anaamini wachezaji anaokwenda nao
wanaweza kumpa ushindi katika mchezo huo wa kirafiki ulio kwenye kalenda ya
Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), kwa sababu amewaandaa vizuri na
wameonyesha wako tayari.
Kim alisema Botswana ni timu nzuri na kwa sasa iko juu ya
Tanzania kiuwezo, hivyo kama wakishinda utawasaidia kupanda kwenye viwango vya
FIFA.
Kim aliwataja wachezaji watakaoondoka alfajiri ni makipa;
Juma Kaseja na Mwadini Ally, mabeki; Aggrey Morris, Kelvin Yondan, Amir Maftah,
Erasto Nyoni, viungo; Athumani Iddi ‘Chuji’, Shaaban Nditi, Salum Abubakar ‘Sure
Boy’, Frank Damayo, Ramadhan Singano ‘Messi’ na Mrisho Ngassa na washambuliaji
Haruna Moshi ‘Boban’, Simon Msuva na Said Bahanuzi.
Kim amesikitika kumkosa mshambuliaji Mbwana Ally Samatta
katika kikosi chake, kwa sababu klabu yake Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo (DRC) haijamruhusu.
“Ni kwa sababu ya siasa kati ya klabu ya Mazembe na TFF,
nasikitika kumkosa Samatta, ila sina jinsi,”alisema.
Kim atamkosa pia mshambuliaji mwingine, John Bocco ‘Adebayor’,
ambaye amekwenda kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa Afrika Kusini
katika klabu ya Super Sport United ya Ligi Kuu ya huko.
Wachezaji watatu kati ya anaokwenda nao Botswana kesho,
Damayo, Singano na Msuva watajiunga na timu hiyo kambini usiku huu, wakitokea
Nigeria walipokuwa na timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro
Heroes.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Angetile Osiah amewataka wachezaji wa Stars kwenda kucheza vizuri huko
ili wazivutie klabu za Kusini mwa Afrika ziwasajili kwa kuwa zina maslahi
makubwa kuliko hapa nchini.
Angetile alisema kwamba Botswana ni nchi ambayo zamani
ilikuwa inasajili wachezaji wa Tanzania, hivyo katika mchezo huo kama wachezaji
wa Stars wataonyesha soka safi, wanaweza kuzivutia klabu za huko na
zikawasajili.
![]() |
| Ngassa na Yondan kulia |
![]() |
| Kazimoto na Maftah kulia |
![]() |
| Nyoni na Redondo kulia |
![]() |
| Sure Boy na Morris kulia |
![]() |
| Boban na Nyoni kulia |
![]() |
| Mwadini na Nditi kulia |
![]() |
| Bahanuz na Dida kulia |
![]() |
| Chuji na Mwadini kulia |
Nahodha Kaseja na Meneja, Lepold Mukebezi 'Taso'












.png)
0 comments:
Post a Comment