• HABARI MPYA

    Thursday, January 10, 2013

    NI TUSKER NA MIEMBENI LEO AMAAN

    Monja Liseki wa Miembeni

    Na Mahmoud Zubeiry
    TUSKER FC inashuka dimbani leo usiku kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar kumenyana na Miembeni katika Nusu Fainali ya pili ya Kombe la Mapinduzi.
    Mchezo huo, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua, kwani kwa sasa Miembeni ndiyo timu inayoiwakilisha vema Zanzibar katika mashindano haya na inaungwa mkono na Wazanzibari wengi.
    Kocha wa Miembeni Salum Bausi amesema hawahofii Tusker na leo atawaonyesha kwamba mpira ni zaidi yua nguvu 
    Nahodha wa Tusker, Joseph Shikokoti amesema kwamba haoni timu ya kuwazuia kutwaa Kombe la Mapinduzi.
    Shikokoti aliyewahi kuchezea Yanga alisema kwamba anafahamu Azam ni wazuri na  watakutana nayo fainali, lakini hawawezi kuwazuia wasitwae Kombe.
    “Hili Kombe letu, tumeona uwezo wa Azam ni wazuri, lakini tutawafunga tukikutana nao, hawana uwezo wa kutuzuia,”alisema Shikokoti.
    Katika Nusu Fainali ya kwanza jana,Azam iliitoa Simba SC kwa penalti 5-4 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 120 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: NI TUSKER NA MIEMBENI LEO AMAAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top