• HABARI MPYA

    Thursday, April 11, 2013

    BARCA CHUPUCHUPU KUAGA, BAYERN YASONGA ILE KIBABE HASWA

    MSHAMBULIAJI Lionel Messi usiku huu ametokea benchi na kuisaidia Barcelona kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kutoa sare ya 1-1 kwenye Uwanja wa Camp Nou na PSG.
    Nyota huyo Argentina, aliyekuwa anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja aliingia kuchukua nafasi ya Cesc Fabregas zikiwa zimesalia dakika 28 huku wageni wakiwa wanaongoza bao 1-0 lililofungwa na Javier Pastore dakika ya 50.
    Lakini Messi alichangia bao la kusawazisha la Barca lililofungwa na Pedro dakika ya 71.
    David Beckham, pia alitokea benchi, akiingia zikiwa zimebaki dakika nane, lakini hakubadilisha matokeo.
    Barca imefuzu kwa faida ya bao la ugenini, baada ya awali kutoa sare ya 2-2 mjini Paris katika mchezo wa kwanza.
    Kikosi cha Barcelona leo kilikuwa: Valdes, Dani Alves, Pique, Adriano/Bartra dk62, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Pedro, Fabregas/Messi dk62 na Villa/Song dk83.
    PSG: Sirigu, Jallet/Van Der Wiel dk88, Alex, Thiago Silva, Maxwell, Lucas Moura, Verratti/Beckham dk83, Thiago Motta, Pastore, Ibrahimovic na Lavezzi/Gameiro dk 81. 
    Game changer: Pedro draw the hosts level after waiting patiently on the edge of the area before firing home
    Bao la kusawazisha: Pedro akiifungia Barca bao lililoipeleka Nusu Fainali
    Game changer: Pedro draw the hosts level after waiting patiently on the edge of the area before firing home
    Stalemate: Gerard Pique joins in on the celebrations after Barcelona's eqauliser against Paris St Germain
    Shangwe: Gerard Pique akiungana na wachezaji wenzake wa Barcelona kushangilia bao la kusawazisha dhidi ya Paris St GermainSuper sub: Lionel Messi started the second leg on the bench but came on for Cesc Fabregas after 62 minutes
    Super sub: Lionel Messi akiingia kuchukua nafasi ya Cesc Fabregas dakika ya 62
    Super sub: Lionel Messi started the second leg on the bench but came on for Cesc Fabregas after 62 minutes
    On target: Dani Alves is unable to stop Javier Pastore as the Argentinian opens the scoring for Paris St Germain
    Anafunga: Dani Alves alishindwa kumzuia Javier Pastore na Muargentina huyo akaifungia bao la kuongoza PSG
    Game on: Barcelona goalkeeper Victor Valdes is unable to stop Pastore's shot as the away side take a surprise lead
    Kitu na boksi: Victor Valdes hakuweza kuzuia mchomo wa Pastore
    Knee-sy does it: Pastore (left) is mobbed by his PSG team-mates after stunning the Nou Camp
    Halikuwa zali lao: Pastore (kushoto) akipongezwa na wenzake wa PSG baada ya kufunga Uwanja wa Nou Camp.
    Star man: But David Beckham started the second leg on the bench before coming on in the 82nd minute
    Mtu nyota: David Beckham akipasha kabla ya kuingia dakika ya 83

    Katika mchezo mwingine, Bayern Munich ilishinda 2-0 ugenini mjini Turin dhidi ya Juventus, hivyo kufuzu kwa jumla ya mabao 4-0.
    Ikichagizwa a ushindi wa awali wa mabao mawili, leo Bayern ilitakataka kutokana na mabao ya Mario Mandzukic dakika ya 64 na Claudio Pizarro dakika ya mwisho.
    Ushindi huu ni mwendelezo wa furaha  kwa Bayern baada ya mwishoni mwa wiki kutwaa taji la 23 la Bundesliga.
    Katika mchezo huo, vikosi vilikuwa;
    Juventus: Buffon, Chiellini, Barzagli, Bonucci, Pogba, Marchisio, Padoin/Isla dk69, Pirlo, Asamoah, Vucinic na Quagliarella/Matri dk66.
    Bayern Munich: Neuer, Dante, Van Buyten/Boateng dk35, Lahm, Ribery, Martinez, Mueller, Alaba, Schweinsteiger, Mandzukic na Robben
    United: Bayern Munich unquestionably deserve their place in the semi-finals

    Umoja: Bayern Munich wakishangilia kutinga Nusu Fainali
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BARCA CHUPUCHUPU KUAGA, BAYERN YASONGA ILE KIBABE HASWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top