• HABARI MPYA

    Wednesday, April 10, 2013

    MESSI AANZA MAZOEZI NA HUENDA AKACHEZA LEO BARCA IKIKIPIGA NA PSG CAMP NOU


    MSHAMBULIAJI Lionel Messi anatarajiwa kurudi uwanjani usiku wa leo, Barcelona ikirudiana na Paris Saint-Germain katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
    Mwanasoka huyo bora wa dunia alikuwa nje kwa wiki mbili baada ya kuumia nyama za paja katika mchezo wa kwanza dhidi ya PSG mjini Paris ambao uliisha kwa sare ya 2-2, hivyo mechi ya Barca ikishinda 5-0 katika La Liga dhidi ya Real Mallorca Jumamosi.
    Pamoja na hayo, klabu imethibitisha alifanya mazoezi na wenzake jana jioni pamoja na mshambuliaji mwingine Pedro  na beki Adriano, ambao pia walikuwa majeruhi.
    "Mchezaji mmoja ambaye yuko chini ya uangalizi wa kocha... ni Leo Messi,"imesema klabu katika tovuti yake.
    Comeback kid: Lionel Messi trained with his team-mates on Tuesday ahead of the PSG match
    Mtoto anarudi: Lionel Messi alifanya mazoezi na wenzake jana kuelekea mechi dhidi ya PSG leo

    Kocha Msaidizi, Jordi Roura, anayemshikia mikoba Tito Vilanova ambaye anaendelea kupata ahueni baada ya kupatiwa tiba ya saratani, amesema Barca itasubiri hadi baada ya mazoezi ya leo kabla ya kuamua kama Messi atacheza au hatacheza.
    Messi amekuwa mfungaji bora katika mashindano ya Ulaya kwa misimu minne iliyopita na msimu huu amekwishafunga mabao manane, lakini anazidiwa mabao matatu na mpinzani wake mkubwa, Cristiano Ronaldo wa Real Madrid ambaye jana alifunga mawili dhidi ya Galatasaray mjini Istanbul.
    Silky: Dani Alves shows off his talents ahead of the second quarter-final leg
    Dani Alves akionyesha kipaji chake mazoezini jana
    Ready: Barcelona have the edge over PSG after scoring two goals in the Paris match
    Tayari: Barcelona wakijifua jana tayari kwa mtanange wa leo

    Ikiwa inajivunia mabao mawili ya ugenini, Barca ina nafasi kubwa ya kuifuata Real Madrid Nusu Fainali kwa mara ya sita na kujiweka sawa katika mbio za kuwania taji la tatu ndani ya miaka mitano.
    Wamecheza mechi 20 za Ligi ya Mabingwa bila kufungwa Nou Camp tangu wafungwe 2-1 na Rubin Kazan, Oktoba mwaka 2009.
    Here they come: Zlatan Ibrahimovic (right) and David Beckham are hoping to upset the odds in Barcelona
    Wanakuja: Zlatan Ibrahimovic (kulia) na David Beckham wana matumaini ya kuiduwaza leo Barcelona
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MESSI AANZA MAZOEZI NA HUENDA AKACHEZA LEO BARCA IKIKIPIGA NA PSG CAMP NOU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top