• HABARI MPYA

    Thursday, June 06, 2013

    FERNANDINHO ATUA MANCHESTER KWA AJILI YA VIPIMO TAYARI KUJIUNGA NA CITY

    IMEWEKWA JUNI 6, 2013 SAA 6:12 USIKU
    KIUNGO Mbrazil, Fernandinho amewasili Kaskazini magharibi kwa ajili ya vipimo vya afya baada ya Shakhtar Donetsk kukubali ofa ya Pauni Milioni 22 kutoka Manchester City.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye ametaka kuhamia Ligi Kuu England ili kuongeza matumaini ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia Brazil mwakani, alipigwa picha katika hospitali ya Bridgewater, Manchester.
    Fernandinho alikuwa ana wasiwasi ndoto zake za kucheza England zingezimwa na klabu yake, Shakhtar.
    On his way: Brazillian midfielder Fernandinho arrives for medical at a Manchester hospital
    Fernandinho akiwasili kwa ajili ya vipimo katika hospitali ya Manchester hospital
    Brazillian midfielder Fernandinho

    UKO WAPI UDHAIFU NA UBORA WA FERNANDINHO?

    Fernandinho ni mpitiaji hodari wa mipira miguuni mwa wapinzani, mwenye kasi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Anacheza vizuri katika ulinzi, lakini pia ni hodari mno katika kuichezesha timu. 
    Si kwamba ana kipaji halisi kama cha Andrea Pirlo, bali ni mzuri katika kumiliki mpira, ana mbinu na maarifa sambamba na hesabu kali kuanzia katika ulinzi hadi kushambulia.
    Mtu ambaye unaweza kumfananisha naye kwa haraka katika soka ya England anaweza kuwa mchezaji wa Chelsea, Mbrazil pia, Ramires, lakini pasi za Fernandinho ni za hatari zaidi kuliko za mwenzake huyo. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: FERNANDINHO ATUA MANCHESTER KWA AJILI YA VIPIMO TAYARI KUJIUNGA NA CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top