• HABARI MPYA

    Tuesday, June 11, 2013

    KIFAA CHA CELTA VIGO CHATUA LIVERPOOL KWA BEI KARIBU NA BURE

    IMEWEKWA JUNI 11, 2013 SAA 9:14 ALASIRI
    MSHAMBULIAJI Iago Aspas anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 7.5 kutua Liverpool baadaye leo, baada ya kufanyiwa vipimo vya afya. 
    Mpachika mabao huyo wa Celta Vigo, ambaye amefunga mara 12 katika La Liga msimu uliomalizika, ameahirisha kwenda mapumzikoni ili kutua Anfield kukamilisha mazungumzo na Wekundu hao. 
    Aspas, mwenye umri wa miaka 25, ambaye aliwasili England jana usiku, alisema: "Nimelazimika kuahirisha safari yangu ya mapumziko Caribbean, lakini sababu ya kufanya hivi naweza kufafanua kwa nini. Wakati niliposikia Liverpool wananitaka sikusita hata kwa dakika moja.'
    Suited and booted: Aspas
    Aspas
    Suti na buti: Iago Aspas anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 7.5 kutua Liverpool leo 
    Iago Aspas
    Iago Aspas
    Karibu Merseyside: Iago Aspas amewasili Liverpool 
    Iago Aspas
     
    "(Liverpool) ni moja ya klabu kubwa duniani na nafikiri nilikuwa nina ofa pia kutoka Italia na Ureno na nchi nyingine, nikaamua mustakabali wangu ni katika soka ya England,"alisema. 
    Klabu hiyo ya Merseyside imekubali kutoa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 7.5 kwa mtumia guu la shoto huyo ambaye ataomba msaada wa wachezaji wenzake kujifunza Kiingereza. 
    "Natumai nitapata msaada kutoka kwa (Jose) Reina, Suso, Dani Pacheco, Luis Suarez, (Philippe) Coutinho, Lucas Leiva na Jose Enrique,"alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KIFAA CHA CELTA VIGO CHATUA LIVERPOOL KWA BEI KARIBU NA BURE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top