IMEWEKWA JULAI 10, 2013 SAA 4:24 ASUBUHI
KIPA Mark Schwarzer amesani Mkataba wa mwaka mmoja Chelsea, baada ya kuondoka Fulham mwishoni mwa msimu kufuatia kumaliza Mkataba wake.
Kipa huyo mwenye umri wa miaka 40 amechezea klabu za Bradford City, Middlesbrough na hivi karibuni Fulham, kwa kipindi cha miaka 17.
"Ni klabu babu kubwa,"alisema kuiambia tovuti ya Chelsea. "Ni moja ya klabu kubwa na bora duniani, na ni heshima kusaini Chelsea. Sikushawishiwa kwa kiasi kikubwa kuja hapa,"alisema.
Kipa mkongwe: Mark Schwarzer amesaini mwaka mmoja Chelsea
Dili limekamilika: Schwarzer akisaini Mkataba wake na Katibu na Mkuruenzi wa klabu, David Barnard
Kipa huyo wa kimataifa wa Australia, ameisaidia nchi yake kufuzu Fainali za Kombe la Dunia Brazil mwakani, na pia atakuwa nyumba ya kipa namba moja Chelsea, Petr Cech, ingawa atapata nafasi ya kuonyesha uwezo wake katika mashindano mbalimbali.
Ameidakia mechi 108 Australia, na mafanikio yake makubwa England ni pamoja na kutwaa Kombe la Ligi akiwa na Middlesbrough mwaka 2003 na kucheza Fainali za KOmbe la UEFA mwaka 2006 na Europa League mwaka 2010.
Utani kidogo: Schwarzer amekutana na nyota wa England, Frank Lampard na John Terry
Akiwa na bosi: Jose Mourinho alikuwa mwenye furaha kumuona kipa mpya
Makipa wamekutana: Schwarzer na kipa mwenzake mpya, Petr Cech
Na huyu rasta: Mshambuliaji wa kimataifa wa Ubelgiji, Romelu Lukaku akiwa na Schwarzer katika viwanja vyao vya mazoezi huko Cobham