IMEWEKWA AGOSTI 18, 2013 SAA 12:10 JIONI
MMILIKI wa Chelsea, Roman Abramovich, ambaye amekuwa hatokeo kuzungumza katika umma au kwenye Vyombo vya Habari, amevunja ukimya wake kwa kwa kutoa shukrani kwa mashabiki wa Chelsea kwa sapoti waliyompa kwa muongo mzima wa kumiliki timu hiyo.
Bilionea huyo Mrusi, ambaye aliichukua timu hiyo Julai mwaka 2003, ameandika ujumbe katika bango la ratiba za mechi kuelekea mchezo wa nyumnani na Hull.
Inasomeka: "Tumekuwa na muongo mzuri pamoja na klabu isingefikia mafanikio haya bila nyinyi. Nawashukuru kwa sapoti, kuna miaka zaidi ya mafanikio.'
Nenda chini kuangalia ukurasa wa ujumbe huo
Wakati wa furaha: Roman Abramovich akiinua taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya la Chelsea mwaka 2012
Muongo wa mafanikio: Abramovich amesaidia kujenga kikosi cha ushindi
Tangu kuwasili kwa Abramovich, klabu hiyo imepitia kwenye mafanikio ambayo haijawahi kupata kabla.
Pamoja na mataji matatu ya Ligi Kuu England, Chelsea pia imetwaa mataji ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, UEFA ndogo maarufu kama Europa League, na Kombe la FA mara nne na Kombe la Ligi mara mbili.
Katika kipindi hicho, ametumia kiasi cha Pauni Milioni 713 kununua wachezaji 72