• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    TFF NAO WAMLILIA RACHEL


    Marehemu Rachel kulia

    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mhariri wa Michezo wa gazeti la Mtanzania, Rachel Mwiligwa kilichotokea leo (Mei 11 mwaka huu) katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam.
    Ofisa Habari wa TFF, Boniphace Wambura ameiambia BIN ZUBEIRY, msiba huo ni mkubwa katika sekta ya habari na mpira wa miguu kwani Rachel kwa kipindi chote akiwa mwandishi na baadaye Mhariri alikuwa akifanya kazi nasi, hivyo mchango wake katika mpira wa miguu tutaukumbuka daima.
    Amesema TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Rachel, kampuni ya New Habari ambayo ndiyo inayomiliki gazeti za Mtanzania na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF NAO WAMLILIA RACHEL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top