![]() |
Marehemu Rachel kulia |
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea
kwa masikitiko kifo cha Mhariri wa Michezo wa gazeti la Mtanzania, Rachel
Mwiligwa kilichotokea leo (Mei 11 mwaka huu) katika Hospitali ya Mwananyamala,
Dar es Salaam.
Ofisa Habari wa TFF, Boniphace Wambura
ameiambia BIN ZUBEIRY, msiba huo ni mkubwa katika sekta ya habari na mpira wa
miguu kwani Rachel kwa kipindi chote akiwa mwandishi na baadaye Mhariri alikuwa
akifanya kazi nasi, hivyo mchango wake katika mpira wa miguu tutaukumbuka
daima.
Amesema TFF inatoa pole kwa familia ya
marehemu Rachel, kampuni ya New Habari ambayo ndiyo inayomiliki gazeti za
Mtanzania na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu
cha msiba huo mzito.
0 comments:
Post a Comment