Yondan anasaini Yanga na mpunga mezani huo |
Na Mahmoud Zubeiry
HIVI unaposoma habari hii,
Simba SC wapo kwenye kikao, kujadili juu ya uamuzi wa kushiriki au kutoshiriki
mchuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama Kombe la Kagame,
iliyoanza leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
Kisa nini? Hawana imani na wenyeji
wa michuano hiyo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) pamoja na Baraza la Vyama
vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECFA). Kivipi? Ni kutokana na kiteno cha vyombo
hivyo kumpa leseni beki wao, Kelvin Patrick Yondan achezee Yanga SC, ambao ni
wapinzani wao wa jadi.
Habari ambazo BIN
ZUBEIRY imezipata kutoka ndani ya Simba SC, zimesema kwamba kitendo cha
Yanga kumchezesha Yondan kwenye klabu hiyo leo, katika mchezo dhidi ya Atletico
ya Burundi, kimeikera sana Simba na kinahisi kuna hujuma wanafanyiwa na TFF na
CECAFA.
Ikumbukwe Yondan aliyejiunga na
Simba 2006, alijiunga na Yanga mwezi uliopita ingawa klabu yake inaendelea
kudai, ina mkataba naye.
BIN ZUBEIRY ilifanikiwa kuwa chombo cha kwanza cha habari duniani
kuonyesha mikataba yote ya Simba na Yanga dhidi ya Yondan.
Lakini Yondan, beki wa kati
hodari nchini, mwenyewe hajawahi hata siku moja kuukana mkataba wowote kati ya
hiyo, zaidi ya kusema kujiunga kwake na Yanga, Simba watajijua wenyewe.
Mwishoni mwa mwaka jana, Yondan
alisusa kuchezea Simba na kuamua kubaki kwao mjini Mwanza, baada ya mechi dhidi
Toto African ya mini humo ya Ligi Kuu.
Na ndipo hapo zilipoanza
kuibuka habari za mchezaji huyo kuhamia kwa watani wa jadi, hadi Mei mwaka huu
alipomwaga wino Jangwani.
Ingawa Yondan kwa sasa yupo kwenye
kambi ya timu mpya, Yanga, lakini klabu yake Simba SC imeendelea kusistiza huyo
ni mchezaji wao halali na sasa inafikiria kujitoa kwenye Kagame baada ya Vidic
wa Tanzania kuchezea Yanga kwenye michuano hiyo.
0 comments:
Post a Comment