• HABARI MPYA

    Saturday, June 09, 2012

    SIMBA YAANZA KULIPA KISASI YANGA, KIGGI ASAINI MIAKA MIWILI


    Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu'
    akionyesha alama ya vidole vitano, kuwakejeli wapinzani wao wa jadi, Yanga
    waliowafunga 5-0 katika Ligi Kuu
    msimu uliopita

    KIUNGO wa Yanga, Kiggi Makassy amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na wapinzani wa jadi, mabingwa wa Tanzania, Simba SC.
    Habari za ndani kutoka kutoka Simba, ambazo BIN ZUBEIRY imezipata kutoka ndani ya Simba, zimesema kwamba, Kiggi ambaye amechoka mwenyewe na maisha ya Yanga, amekwenda Simba kwa hiari na mapenzi yake.
    Kiggi ambaye mjomba wake, Itutu Kiggi ‘Road Master’ aling’ara Simba mwaka 1991 akiiwezesha timu hiyo kutwaa Klabu Bingwa Afrika Mashariki, msimu huu haukuwa mzuri kwake Yanga, kutokana na kuwekwa benchi mfululizo.
    Kiggi ni mchezaji mzuri, ambaye siku za karibuni Yanga walishindwa kumtumia vizuri na kuonekana kama ameshuka kisoka, lakini kuna matumaini makubwa atang’ara Simba.
    Kiggi Makassy
    Historia inaonyesha wachezaji wengi wanaoondoka Yanga kwenda Simba, hung’ara - kuanzia enzi za Ezekiel Greyson ‘Jujuman’, Said Mwamba ‘Kizota’ (wote marehemu), Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Mohamed Banka na Amiri Maftah.   
    Kiggi alijiunga na Yanga mwaka 2008, akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro, ambayo nayo ilimtoa kituo cha kukuza vipaji cha Rollingston cha Arusha, kinachomilikiwa na mwanasoka wa zamani wa kimataifa nchini, Ally Mtumwa. 
    Tayari Yanga imesajili wachezaji wawili wa Simba, ambao ni kipa Ally Mustafa 'Barthez' na beki Kelvin Yonda, hivyo Simba sasa ni kama inaanza kulipa kisasi. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA YAANZA KULIPA KISASI YANGA, KIGGI ASAINI MIAKA MIWILI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top