• HABARI MPYA

    Saturday, June 09, 2012

    DEFOE AREJEA KIKOSINI ENGLAND BAADA YA KUMZIKA BABA YAKE


    Jermain Defoe arrives back at England's team hotel
    AMEREJEA... Jermain Defoe akiwasili katika hoteli waliyoweka kambi England
    Published: 29 minutes ago

    JERMAIN DEFOE amerejea kwenye kambi ya timu ya taifa ya England asubuhi ya leo akitoka kwenye mazishi ya baba yake mzazi.

    Mshambuliaji huyo wa Tottenham, alirejea nyumbani Alhamisi asubuhi baada ya kupata habari hizo za kuhuzunisha.
    Pamoja na hayo amejiunga tena na wenzake kambini majira ya saa 3 asubuhi na alitarajiwa kushiriki mazoezi katika Uwanja ambao mashabiki hawataruhusiwa kuingia.
    England inajiandaa kwa mechi ya ufunguzi ya Kundi D Jumatatu dhidi ya Ufaransa mjini Donetsk.
    Kocha Roy Hodgson anafurahia kurejea kjwa Defoe kikosini.
    Pamoja na hayo, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29, hatarajiwi kuanza Jumatatu dhidi ya Ufaransa.
    Ashley Young anatarajiwa kuchukua nafasi ya ushambuliaji, katika mechi hiyo badala ya Wayne Rooney anayetumikia adhabu.
    BACK IN THE FOLD ... Jermain Defoe
     ... Jermain Defoe
    Andy Carroll na Danny Welbeck wanatarajiwa kuwa washambuliaji wengine  pamoja na mshambuliaji huyo wa Manchester United.
    Carroll alicheza pamoja na  Young katika mazoezi ya wazi jana.
    Pamoja na hayo, mshambuliaji huyo wa  Liverpool alikuwa mmoja wa waliotembelea Auschwitz na FA jana.
    Jermain Defoe leaves for training with the rest of the England squad
    SAFARI ... Jermain Defoe akitoka mazoezini 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DEFOE AREJEA KIKOSINI ENGLAND BAADA YA KUMZIKA BABA YAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top