• HABARI MPYA

    Sunday, November 18, 2012

    SERENGETI BOYS NA KONGO KATIKA PICHA LEO TAIFA

    Kipa wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, ya Kongo Brazzaville, Ombandza Mpea Joe akilalama baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Mufathir Yahya Abbas kutinga nyavuni na kuwapa wenyeji ushindi wa 1-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni ya leo.

    Bao pekee leo

    Kipa wa Kongo akining'inia kwenye milingoti ya lango baada ya kuukosa mpira uliopaa juu ya lango lake

    Mchezaji wa Serengeti, Suleiman Hamisi Bofu akipiga mpira kichwa mbele ya beki wa Kongo, Ondongo Boungena

    Beki Okombi Francis wa Kongo akiokoa mbele ya Joseph Kimwaga 

    Wachezaji wa Kongo wakimdhibiti mchezaji wa Serengeti

    Hussein Twaha 'Messi' akiwafunga tela wachezaji wa Kongo

    Makocha wa Serengeti Jacob Michelsen na Msaidizi wake Jamhuri Kihwelo wakiwapa maelekezo vijana wao wakati mpira uliposimama kwa muda

    Kipa wa Serengeti Boys, Peter Manyika akiruka hewani kupangua mchomo mkali ulioelekezwa langoni mwake 

    Kipa wa Kongo, akimdondokea kiungo wa Serengeti, Farid Mussa Shah kudaka mpira, huku beki wake, Ondongo Boungena akiwa tayari kumsaidia 

    Farid kulia na Ondongo kushoto

    Kikosi cha vijeba wa Kongo Brazzaville

    Beki Ismail Adam Gambo wa Serengeti akimdhibiti Ibara Vinny wa Kongo Brazzazille

    Hussein Twaha akiwatoka wachezaji wa Kongo

    Serengeti wakishangilia bao lao kwa staili ya aina yake

    11 wa kwanza wa Serengeti leo

    Wachezaji wa Serengeti Boys wakiimba wimbo wa taifa

    Benchi la Ufundi la Serengeti Boys wakati wa wimbo wa taifa

    Hussein Twaha akipasua katikati ya msitu wa wachezaji wa Kongo

    Hussein Twaha akimiliki mpira mbele ya beki wa Kongo

    Joseph Kimwaga akimtoka beki wa Kongo Brazzaville


    Beki wa Kongo Okombi Francis baada ya kumpitia kwanja Tumaini Baraka Mosha wa Serengeti
    Mudathir akiondoka na mpira

    Tumaini Baraka Mosha akimtoka Okombi

    Kushoto refa anasema twende, huku Tumaini Baraka Mosha akiwania mpira dhidi ya Ondongo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: SERENGETI BOYS NA KONGO KATIKA PICHA LEO TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top