• HABARI MPYA

    Saturday, May 12, 2012

    AKINA SAMATTA SASA SHWARI, WANACHEZA LEO NA MERREIKH


    Des Corbeaux appliqués au "château rouge"
    Mazembe wakijifua Uwanja wa Marreikh jana, tayari kwa mchezo wa leo


    Mazembe wakiwasili uwanja wa Merreikh...
     HATIMAYE hali imekuwa shwari kwa Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), baada ya jana walipowasili mjini Khartoum kupokewa kwa kushambuliwa hadi basi lao kupasuliwa vioo.
    Mechi baina yao na wenyeji El Merreikh ya Sudan, hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika inafanyika leo usiku.
    Mazembe yenye washambuliaji wawili wa Kitanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu jana usiku ilifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Merreikh.
    Walitumia daika 22 ili kuuzoea Uwanja huo, kuanzia saa 1:40 usiku kwa saa za huko. Uwanja ulikuwa umepambwa kwa rangi za wapinzani wao, Merreikh nyekundu na njano.
    Tayari kocha Lamine amekwishateua wachezaji 18 wa kushiriki mchezo huo, kati ya 22 aliokwenda nao.
    Hao ni makipa: KIDIABA na MATAMPI - mabeki: NKULUKUTA, KIMWAKI, Mihayo, HICHANI, KASUSULA, Sunzu, na NDONGA KASONGO - viungo: Sinkala, Ochan, Ilongo, Kalaba, MPUTU, na LUSADISU Kasonde – wakati washambuliaji ni Singuluma, SAMATA, LUNGU, Traore na KANDA.
    Katika mchezo wa kwanza, Mazembe ilishinda 2-0 nyumbani, Samatta akifunga bao moja na leo inahitaji hata sare ili kusonga mbele.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AKINA SAMATTA SASA SHWARI, WANACHEZA LEO NA MERREIKH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top