• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    BARCA YAMSAFISHA MESSI KASHFA YA UBAGUZI


    Lionel Messi
    Lionel Messi
    Everton midfielder Royston Drenthe
    Drenthe

    KLABU ya Barcelona imemtetea Lionel Messi dhidi ya tuhuma za ubaguzi alizotupiwa na Royston Drenthe.
    Mholanzi Drenthe, ambaye kwa sasa anachezea Everton kwa mkopo, akitokea Real Madrid, alidai Messi alimuita "negro" mara kadhaa wakati akicheza Hispania.
    Barcelona imeyapuuza madai hayo na kusema Messi hana tabia hiyo.
    "Mchezaji huyo wakati wote amekuwa akionyesha heshima kwa kiwango kinachotakiwa na uanamichezo kwa wapinzani wake," alisema Msemaji wa Barca.
    Drenthe mwenye umri wa miaka 25, akiwa katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake Real Madrid, msimu huu amecheza kwa mkopo Goodison Park, lakini hivi karibuni alienguliwa kwenye kikosi cha David Moyes kwa utovu wa nidhamu.
    Alijiunga na Real akitokea Feyenoord mwaka 2007 na msimu uliopita alichezea kwa mkopo Hercules ya Hispania.
    Pamoja na kumuita negro mara kadhaa, Drenthe alidai mara ya mwisho alipokutana uwanjani na Messi, pia aligoma kupeana naye mikono baada ya mechi.
    Jana, Ligi Kuu ya Hispania, Primera Liga ilisema haijapanga kumchukulia hatua Messi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCA YAMSAFISHA MESSI KASHFA YA UBAGUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top