![]() |
| John Bocco kushoto, akiwa Said Mourad kulia aliyeshinda tuzo ya mchezaji aliye fiti zaidi Azam msimu huu |
JOHN Raphael Bocco maarufu kama Adebayor
leo amefunga bao moja katika ushindi wa 2-1 wa Azam katika mechi ya mwisho ya
Ligi Kuu dhidi ya Kagera Sugar na kutwaa kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara kwa kufikisha mabao 19.
Bocco amempiku mshambuliaji wa Simba,
Emmanuel Okwi aliyemaliza na mabao 12 na hivyo kufanya kiatu cha dhahabu cha
Ligi Kuu kiweke maskani Chamazi kwa msimu wa pili mfululizo, kwani msimu
uliopita alitwaa mchezaji wa Azam pia, Mrisho Ngassa.
Azam pamoja na kumpongeza Bocco kwa mchango
wake huo mkubwa uliowezesha klabu kushika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu, pia
wamemtangaza kwamba ndiye mchezaji bora wa msimu wa klabu hiyo.
Akizungumza katika hafla ya kuwapongeza
wachezaji wa timu hiyo, iliyofanyika hoteli ya JB Belmonte katikati ya Jiji, Mwenyekiti
wa Azam FC, Abubakar Bakhresa alisema kwamba wanampongeza Bocco kwa mchango
wake na wanamuomba aongeze juhudi.
Awali kwenye hafla hiyo, Katibu Mkuu wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Agetile Osiah Malabeja alisema kwamba
wanavutiwa sana na Bocco kwa nidhamu yake na kujituma- lakini akamuomba
abadilishe uamuzi wake wa kujiuzulu kuchezea timu ya taifa ya Tanzania, Taifa
Stars kwa sababu yeye bado ni kijana mdogo na taifa linahitaji mchango wake
bado.
Bocco alifikia uamuzi wa kujiuzulu Stars
kutokana na kuzomewa na mashabiki kwa sababu anakosa sana mabao.
Lakini wadau wengi wamekuwa wakimsihi
abadilishe uamuzi wake na kurejea kwenye timu- ili afanyie kazi mapungufu yake
na siku moja atakuwa kinara wa mabao wa timu.



.png)
0 comments:
Post a Comment