• HABARI MPYA

    Monday, May 07, 2012

    KASEJA AVUNJA REKODI YA PAZI


    Kaseja

    JUMA Kaseja, kipa wa SImba SC leo amevunja rekodi ya kipa wa zamani wa timu hiyo, Iddi Pazi ‘Father’ ya kufunga bao dhidi ya watani wa jadi, Yanga.
    Pazi alifunga kwa penalti mwaka 1984 katika sare ya 1-1 na Yanga, wakati leo Kaseja amefunga bao la nne, Simba ikiifunga Yanga 5-0 Uwanja wa taifa, Dar es Salaam.
    Mwameja Mohamed ni kipa mwingine aliyewafunga Yanga kwa penalti, lakini yeye alifunga baada ya dakika 120 za sare.
    Kaseja anaelekea kuweka rekodi ya kuwa kipa bora wa kihistoria kuwahi kutokea SImba, kwani akiwa katika mwaka wake wa tisa tangu ajiunge na klabu hiyo mwaka 2003 bado yuko juu na bado anaibeba timu.   
    Japokuwa Simba wamepita makipa wengi bora, wakiwemo Omar Mahadhi ‘Bin Jabir’, Athumani Mambosasa (wote marehemu) na Iddi Pazi, lakini kwa sasa Mwameja ndiye aliyeiletea mafanikio makubwa zaidi timu hiyo, akiifikisha fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993 na kuipa mataji manne ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, 1992, 1995, 1996 na 2002.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KASEJA AVUNJA REKODI YA PAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top