• HABARI MPYA

    Thursday, May 10, 2012

    HAWA NDIO WAZEE WENU WANA YANGA, KILA KUKICHA MIZENGWE NA FITINA, JE MTAFIKA?


    WAZEE wa klabu ya Yanga, wakiongozwa na ‘kinara wa migogoro’ klabuni, Mzee Ibrahim Akilimali, ambaye rekodi zinaonyesha hakubaliki Yanga, kwa sasa wanampiga zengwe Mwenyekiti wa klabu hiyo, Wakili Lloyd Baharagu Nchunga.
    Mzee Akilimali historia inaonyesha hakubaliki Yanga, kwa sababu mwaka 1993 alitaka kugombea Uenyekiti, lakini alipofika kwenye ukumbi wa mkutano, Uwanja wa Ndani wa Taifa, alipoona joto la uchaguzi huo kwamba hakubaliki alitaka kujitoa ili awanie Umakamu Mwenyekiti na huko pia wakamzuia kugombea.
    Wazee hawa ambao wanatamba kwenye vyombo vya habari wakimpiga vita Nchunga, historia inaonyesha wamekuwa bughudha kwa uongozi wa klabu, si wakati huu tu wa Nchunga, bali hawa ndio waliompindua mzee mwenzao, marehemu Rashid Ngozoma Matunda (Mwenyezimungu amrehemu), kabla hawajagonga mwamba kwa jemedari, Wakili Imani Omar Madega, ambaye aliwapsha na wakarudi nyuma na kumuacha aongoze klabu, hadi muda wake ulipofika akaachia madaraka kwa amani, tena akishangiliwa na wana Yanga PTA.
    Madega aliwashushia kauli nzito, akisema; “Wazee na wanachama wachache waroho wa Yanga, kuweni macho na msiwasaliti wazee wenzenu, ambao walifanya juhudi kuifanya Yanga iwe na jina kubwa, mkiendelea kufanya hivyo kwa hakika historia itawahukumu, uongozi uko imara kutetea maslahi ya Yanga,”.
    Madega aliwapa dongo hili, wakati wazee hao walipokuwa wakidaiwa kutumiwa na tajiri mmoja ili kumpindua Madega, kwa sababu hakuwa tayari kufuata matakwa ya tajiri huyo.
    Kauli hii, Madega aliitoa Oktoba 11, mwaka 2007 mjini Dar es Salaam.
    Sasa, Wazee hawa tena, wanampiga zengwe Nchunga, je kwao nani atafaa kuongoza Yanga? Tujadili.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HAWA NDIO WAZEE WENU WANA YANGA, KILA KUKICHA MIZENGWE NA FITINA, JE MTAFIKA? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top