• HABARI MPYA

    Thursday, May 10, 2012

    MAN CITY, MAN UNITED NA CHELSEA ZAGOMBEA SAINI YA DEMBELE


    Moussa Dembele, Fulham (Getty Images)
    Dembele


    KLABU za Manchester United, Manchester City na Chelsea zimeungana katika mbio za kuwania saini ya kiungo na mshambuliaji Moussa Dembele wa Fulham, BIN ZUBEIRY ameipata hiyo.
    Mpachika mabao huyo amekuwa akifuatiliwa na klabu zote kubwa za Ligi Kuu England, ili kupata saini yake.
    BIN ZUBEIRY imepata habari kutoka Goal.com kwamba Machi, mwaka huu Arsenal, Liverpool na Tottenham zilikuwa zinamfuatilia kwa karibu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24.
    Na mwansoka huyo wa kimataifa wa Ubelgiji, ametoa mchango mkubwa kwa Fulham hadi inashika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Ligi Kuu msimu huu, jambo ambalo limezifanya klabu kubwa zimsake kwa ofa ya mshahara mnono.
    Thamani ya Dembele inakadiriwa kuwa kati ya pauni Milioni 12 hadi 15 ambazo Fulham, inaweza kupokea kumuuza.
    Pamoja na hayo, Dembele ana mwaka mmoja tu zaidi katika mkataba wake wa sasa na Fulham na hata kumuuza kwa dau la pauni Milioni 10 itakuwa sawa tu.
    Lakini Fulham yenyewe iko tayari kukubaliana mkataba mpya na mchezaji huyo, ambaye walimchukua kutoka AZ Alkmaar ya Uholanzi kwa daua la puni Milioni 5 mwishoni mwa msimu wa 2010.
    Lakini klabu hiyo ya London, ambayo mchezaji ghali kwao ni kipa Mark Schwarzer, inajua haiwezi kushindana na vigogo vya England katika suala la ofa ya mshahara mnono kwa mchezaji huyo.
    Dembele anachukuliwa kama moja ya rasilimali mbili muhimu Fulham za bei mbaya, mwingine akiwa ni Clint Dempsey, ambaye mustakabali wake klabuni hapo naye uko shakani, akiwa amebakiza mwaka mmoja kumaliza mkataba wake. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY, MAN UNITED NA CHELSEA ZAGOMBEA SAINI YA DEMBELE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top