• HABARI MPYA

    Sunday, May 06, 2012

    HAYE, CHISORA ULINGONI JULAI 14


    David Haye
    SHOWDOWN ... Chisora walipozinguana Munich
    Published: 05th May 2012
    DAVID HAYE atarejea ulingoni kutoka kwenye kustaafu kwa kuzipiga na Dereck Chisora Julai 14, mwaka huu.

    Promota Frank Warren anatarajiwa kutangaza pambano hilo Jumanne kwenye Uwanja wa Upton Park, ambako linatarajiwa kufanyika pambano la uzito wa Light kwa Ricky Burns kutetea ubingwa wake wa dunia dhidi ya Kevin Mitchell.
    Lakini pambano la Haye-Chisora linaweza kuendelea japokuwa Chisora amepokonywa leseni.
    Suluhisho pekee ni kwa Warren ni kufanyia pambano hilo nje ya nchi hiyo.
    Haye na Chisora bifu lao maarufu liliibuka mjini Munich Februari katika mkutano na waandishi wa habari baada ya pambano la Chisora na Vitali Klitschko, baada ya kuzipiga kavukavu.
    Chisora ndiye aliyeanza kumzaba kibao bingwa huyo wa WBC, hivyo akafungiwa na Bodi ya Udhibiti.
    Haye aliepuka adhabu hiyo kwa sababu alikuwa amekwishatangaza kustaafu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HAYE, CHISORA ULINGONI JULAI 14 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top