• HABARI MPYA

    Sunday, May 06, 2012

    NGORONGORO KUIVAA NIGERIA BAADA YA KUITOA SUDAN


    Ulimwengu, mfungaji wa bao la Ngorongoro

    TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes imefanikiwa kusonga mbele katika kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika usiku huu, baada ya kutioa Sudan kwa jumla ya mabao 4-3.
    Ngorongoro leo imekubali kichapo chepesi cha mabao 2-1 ugenini, kwenye Uwanja wa Khartoum, baada ya awali kushinda 3-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wiki mbili zilizopita na sasa itachuana na Nigeria Raundi ya Pili, mechi ya kwanza ikicheza Julai 28, mwaka huu Dar es Salaam.
    Sudan walipata mabao yao kupitia kwa Mohammed Abdelrahman dakika ya 10 na Ahmad Nasr kwa penalti dakika ya 65, wakati bao la Ngorongoro lilifungwa na mshambuliaji wa Tout Puissant  Mazembe ya DRC, Thomas Emmanuel Ulimwengu kabla ya mapumziko.
    Ngorongoro Heroesinatarajiwa kurejea nchini Jumapili (leo) majira ya Saa 3 asubuhi.
    Mshindi kati ya Ngorongoro na Nigeria atamenyana na mshindi kati ya Afrika Kusini na Kongo Brazzaville, mechi ya kwanza ikichezwa kati ya Septemba 21 na 23 mwaka huu ugenini na marudiano Oktoba 6.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NGORONGORO KUIVAA NIGERIA BAADA YA KUITOA SUDAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top