MCHEZA filamu anayetamba kwenye ‘game,’
Jacob Steven ‘JB’ (pichani) hivi karibuni alinusurika kuuawa na majambazi
waliovamia Pub ya msanii mwenzake, Aunt Ezekiel iliyopo eneo liitwalo Gereji
Mwananyamala jijini Dar.
Akizungumza na gazeti la Ijumaa, JB alisema kuwa
baada ya majambazi hao kuvamia katika pub hiyo saa 5.30 usiku, hakuwastukia
kama walikuwa wahalifu bali alidhani ni wateja wa kawaida.
“Mimi sikuwashitukia kama wale watu
walikuwa majambazi, ila baada ya kutoa bastola na kutuamuru tulale chini na
tutoe kila kitu nikajua kimenuka, nikatimua mbio ambazo sijawahi kukimbia licha
ya mwili wangu huu,” alisema JB.
Aliongeza kuwa, wakati akitimua mbio
aliwasikia watu wakimuaru asimame lakini hakutii hadi alipofika Kituo cha
daladala cha Komakoma ndipo alisimama na kumshukuru Mungu kwa kumnusuru na
kifo.


.png)
0 comments:
Post a Comment