• HABARI MPYA

    Friday, May 04, 2012

    KABURI LA KANUMBA LAKARABATIWA


    kabuli la kanumba lililoibwa mashada
    Na,Shakoor Jongo
    ‘ICON’ katika tasnia ya filamu Bongo, Irene Uwoya na mwenzake Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ hivi karibuni walimtafuta fundi na kwenda kulifanyia ukarabati kaburi la staa mwenzao marehemu Steven Kanumba.
    Akizungumza na Ijumaa mmoja wa watu wanaojihusisha na kazi ya uchimbaji makaburi eneo la Kinondoni Dar, aliyejitambulisha kwa jina la Kidevu, alisema Ijumaa ya wiki iyopita alishuhudia mafundi wakilikarabati kaburi hilo huku Uwoya na Steve wakiwa pembeni.
    “Baada ya lile kaburi kupasuka na kuanza kutitia, juzi niliwaona mafundi wakilikarabati huku pembeni wakiwa wamesimama waigizaji wawili yule mfupi anayeiga sauti ya Nyerere na Uwoya,” alisema Kidevu.
    Akizungumzia hilo, Steve Nyerere alisema:
    “Ni kweli mimi na Irene tuliamua kulikarabati kaburi la Kanumba baada ya kusoma gazetini kwamba limeanza kutitia.

    GAZETI LA IJUMAA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KABURI LA KANUMBA LAKARABATIWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top