• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    MAJAMBAZI WAICHELEWESHA SIMBA SUDAN


    Wachezaji wa Simba wakishangilia ubingwa wao

    KIKOSI cha Simba kinagtarajiwa kuondoka leo mchana kwenda Sudan kupitia Nairobi, Kenya tayari kwa mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy baada ya kukwama kuondoka kutokana na majambazi kuvunja na kuiba katika ubalozi wa Sudan.
    Juzi usiku majambazi walivunja sefu ya kuhifadhia fedha na kuiba zaidi ya dola 40,000 ubalozini hapo pamoja fedha nyingine pamoja na kuiba kompyuta zote zinazotumika kuhifadhia kumbukumbu mbalimbali.
    Kutokana na hali hiyo, Simba walikwama kupata viza zao juzi na jana na zinataraji kutolewa leo asubuhi kabla ya kuondoka saa 10:00 kwenda Sudan kupitia Nairobi ikiwa na wachezaji wote wa timu hiyo.
    Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alithibitisha juzi kutokea tukio hilo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAJAMBAZI WAICHELEWESHA SIMBA SUDAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top