• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    OKWI, SUNZU AFRIKA YAWATAMBUA, YANGA SHIKENI ADABU


    Okwi

    WAKATI wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho, Simba wakiondoka leo kwenda Khartoum, Sudan tayari kwa mchezo wa marudiono dhidi ya Al Ahly Shendi,  washambuliaji nyota wa Wekundu hao wa Msimbazi, Emmanuel Okwi na Felix Sunzu wameingia kwenye rekodi ya wafungaji bora Afrika katika michuano ya Kombe la Shirikisho la soka Afrika.
    Gazeti la Mwananchi leo, limeandika kwamba Okwi, raia wa Uganda na Felix Sunzu ambaye ni Mzambia, wote wametajwa kuwa na mabao matatu kila mmoja kwa mujibu wa mtandao wa tensport.com.
    Mshambuliaji huyo anayechezea pia Uganda Cranes, alifunga bao moja dhidi ya Entente Sportive de Setif katika mchezo wa kwanza kati ya mawili walioshinda mabao 2-0 Dar es Salaam na moja likifungwa na Haruna Moshi.
    Mchezo wa marudiano, Okwi alifunga moja wakati Simba ikilala mabao 3-1. Mshambuliaji huyo alifunga dhidi ya Al Ahly Shendi kati ya mabao matatu huku mengine yakifungwa na Boban na Patrick Mafisango.
    Kwa hali hiyo, Boban na Sunzu kila mmoja wana mabao matatu. Sunzu aliyafunga katika mchezo walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Kiyovu ya Rwanda na lingine likifungwa na Parick Mafisango.
    Mbali na wachezaji hao, wengine wenye mabao matatu ni Komara, Niamba wote wa Leopards ya Congo, Chinyengetere (Hwange ya Zimbabwe, Moco (InterClube (Angola) na Raouf (ENPPI, Misri) na Seri wa Asec Mimosa ya Ivory Coast.
    Mpaka sasa Fiston (Lydia Academic, Burundi) na Girma wa St George ya Ethiopia wana mabao manne kila mmoja.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: OKWI, SUNZU AFRIKA YAWATAMBUA, YANGA SHIKENI ADABU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top