• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    SHEIKH MANSOUR ATOA OFA KUFURU MAN CITY IKITWAA UBINGWA


    Wachezaji wa Man City wakipongezana katika moja ya mechi za Ligi Kuu walizoshinda msimu huu

    BILIONEA na mmiliki wa klabu ya Manchester City, Sheikh Mansour amewaahidi wachezaji wake posho nene ya Sh600 milioni (sawa na pauni 250,000) kila mchezaji iwapo watafanikiwa kuipiku Manchester United na kutwaa ubingwa.
    Kikosi cha Kocha Roberto Mancini kiko jirani zaidi na kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa England kwa mara ya kwanza tangu ilipofanya hivyo mara ya mwisho mwaka 1968.Tajiri Mansour anaamini zawadi ya ubingwa wa England haitoshi kuwafurahisha wachezaji wake, kwa maana hiyo amekubali kuzama mfukoni mwake na kutoa ziada ili kuwapa wachezaji wake.
    Kwa mujibu wa gazeti la 'The Daily Star', bosi Mansour amewaambia wachezaji wake kama wanataka pesa, basi wahakikishe wanatwaa ubingwa msimu huu.
    Man City inamaliza msimu wa ligi kwa kuvaanana timu ya Queens Park Rangers kwenye Uwanja wa Etihad Jumapili inayofuata, na ili iweze kuweka rekodi hiyo mpya italazimika kuifunga QPR inayohitaji pointi ili ibaki Ligi Kuu msimu ujao.
    Taarifa zaidi zinadai kuwa bilionea huyo yuko tayari kumwaga kiasi cha pauni 4.5milioni (Sh11.3 bilioni) kama motisha kwa timu nzima.
    Manchester United inahitaji miujiza kutetea taji msimu huu pamoja na kwamba wanalingana kwa pointi na City, lakini wapinzani wao wana utajiri wa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.Ni ushindi tu utakaowapa rekodi mpya ya kutwaa ubingwa wa England walioutafuta kwa zaidi ya miaka 42. United wanamaliza ligi kwa kuvaana na Sunderland.
    Wakati City wakiandaliwa bonas hiyo iwapo watatwaa ubingwa, timu ya Blackburn imeshuka rasmi daraja baada ya usiku wa kuamkia jana kufungwa bao 1-0 kwenye uwanja wa nyumbani dhidi ya Wigan.
    Blackburn ilikuwa ikihitaji ushindi ili ijinusuru na anguko hilo, lakini walijikuta wakipoteza mchezo huo mbele ya mashabiki wao dhidi ya timu ambayo tayari ina uhakika wa kucheza ligi msimu ujao.
    Bao lililoizamisha Rovers lilifungwa kwa kichwa na Antolin Alcaraz aliyemaliza mpira wa kona uliochongwa na Latics ndani ya dimba la Ewood Park.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SHEIKH MANSOUR ATOA OFA KUFURU MAN CITY IKITWAA UBINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top