![]() |
| Owen Kasule |
KIUNGO wa timu ya Taifa ya Uganda ‘The
Cranes’, Owen Kasule ametua Dar es Salaam kufanya mazungumzo ya usajili na
uongozi wa timu ya Yanga ya Dar es Salaam.
Gazeti la Habari Leo, limeandika kwamba Kasule
alifika Dar es Salaam juzi, ambapo jana alifanya mazungumzo ya muda mrefu na
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga inayoongozwa na Salum Rupia kuhusiana
na
kusajiliwa na timu hiyo kwa ajili ya Ligi
Kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Habari zilizopatikana ndani ya Yanga jana
na kuthibitishwa na Rupia pamoja na Kasule zilieleza kuwa mazungumzo hayo
yalikuwa mazuri, lakini kuna mambo ya kimsingi ambayo yaliwakwamisha kufikia
mwafaka.
Rupia alikiri kuzungumza na Kasule jana,
lakini alisema hawakusaini naye mkataba kwani amewaambia anaenda kufanya
majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika timu ya Al Ahly ya Misri na kwamba
kama atakwama huko atakuja kusaini Yanga.
Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Usajili
alisema, Kasule amewaeleza kuwa ni rafiki wa karibu wa mshambuliaji Hamisi
Kiiza wa Yanga na Emmanuel Okwi wa Simba ambao amesoma nao shule Uganda, hivyo
wanapomjulisha habari za soka la Tanzania anatamani sana kuja kucheza.
“Ametwambia ana mapenzi sana na Yanga,
hivyo naamini atakuja,” alisema Rupia. Okwi na Kiiza ni miongoni mwa wachezaji
wa nje waliong’ara kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika Jumapili.
Kwa upande wake Kasule akizungumza jana
akiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kabla ya kurejea kwao, alikiri
kuzungumza na Yanga, lakini akisema kuna mambo hawajafikia mwafaka.
“Mazungumzo yetu hayajaisha, nitakujulisha
kwa kirefu zaidi, lakini kwa sasa hapana, elewa kwamba tumezungumza na Yanga,”
alisema.



.png)
0 comments:
Post a Comment