• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    TAIFA QUEENS YAANZA VEMA AFRIKA


    Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano wa SBL, Teddy Mapunda akizungumza na Henry Tandau katika ufunguzi wa michuano ya Afrika ya Netoboli, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. mbele kabisa ni Ofisa mwingine wa SBL, Nandi. 

    Wa wa Taifa Queens michuano ya Afrika ya Netoboli, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 








    TIMU ya Taifa ya netiboli ya Tanzania (Taifa Queens), jana ilianza vizuri mashindano ya mchezo huo ya Afrika yanayofanyika jijini Dar es Salaam baada ya kutoa kipigo kizito kwa Lesotho cha mabao 57-13.
    Taifa Queens tangu mwanzo walionekana kupania kufanya vizuri katika mchezo huo ambao mgeni rasmi alikuwa mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
    Hadi robo ya kwanza inamalizika, Taifa Queens walikuwa mbele kwa mabao 13-3 na kuendelea
    kuwachachafya wapinzani wao na kumaliza robo ya tatu wakiendelea kuongoza kwa 40-13.
    Wakicheza kwa uelewano mkubwa, Taifa Queens iliyopiga kambi kwa takribani miezi mitatu katika Shule ya Sekondari ya Filbert Bayi Kibaha, ilizidi kuwapeleka puta wapinzani wao ambao hawakufunga hata bao moja katika robo ya mwisho.
    Akizungumza wakati wa ufunguaji wa mashindano hayo, Mama Salma Kikwete alisema mashindano hayo yasaidie kukuza ushirikiano miongoni mwa nchi za Afrika.
    Alitoa wito kwa viongozi wa michezo na taasisi za mahusiano ya kimataifa katika nchi za Kiafrika kutumia vizuri fursa za michezo katika kukuza na kuboresha mahusiano ya nchi za Afrika.
    Naye Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara alivitaka vyama vya michezo kujipanga vizuri ili kuhakikisha vinafanikisha malengo yao .
    Mashindano hayo yanayoshirikisha nchi saba yanaendelea tena leo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na hakuna kiingilio.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA QUEENS YAANZA VEMA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top