![]() |
TIMU ya taifa ya netiboli ya Tanzania
‘Taifa Queens’ jana ilishindwa kujisafishia njia baada ya kukubali kipigo cha
mabao 33-30 dhidi ya mabingwa watetezi Malawi katika michuano ya mchezo huo ya
Afrika.
Katika mchezo huo mkali na wa kuvutia,
uliofanyika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, timu zote mbili zilitumia nguvu na
ufundi wa hali ya juu.
Malawi walianza kwa kasi mchezo huo na
kuwaongoza wenyeji kwa magoli 13-6 katika robo ya kwanza.
Baada ya kuona hivyo, kocha wa Tanzania,
Mary Protas alilazimika kufanya mabadiliko robo ya pili kwa kumtoa mfungaji
mrefu zaidi na Mwanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2011 Mwanaidi Hassan na
kumuingiza Pili Peter nafasi ya ufungaji (GS).
Mabadiliko hayo yalikuwa ya kiufundi
kutokana na Mwanaidi kutoelewana vema mfungaji msaidizi (GA), Irene Elias na
yalizaa matunda hivyo timu kwenda mapumziko ikiwa nyuma kwa mabao 19-12.
Baada ya mapumziko Tanzania ilifanya
mabadiliko mengine kwa kumtoa Irene na kumuingiza Mwadawa Twalib kusaidiana na
Pili katika ufungaji.
Kadri mchezo ulivyosonga Taifa Queens
ilionekana kuzinduka zaidi na kuwabana wapinzani wao hivyo hadi robo ya tatu
kuendelea kubaki nyuma kwa tofauti ya magoli saba ambayo
waliruhusu robo ya kwanza na kuwa nyuma kwa
27-20.
Mabadiliko ya robo ya mwisho ya kumtoa Pili
katika GS na kurudi Mwanaidi na Paskazia Kibayasa kuingia WD badala ya Restuta
Boniface yalizaa matunda na hivyo kumaliza mchezo kwa mabao 34-30.
Hata hivyo, kocha wa Tanzania, Protas
alimlalamikia mwamuzi kutoka Lesotho, Chakatsa Lephole kuwa chanzo cha kipigo
kwa timu yake hivyo kuwaacha njia panda katika mbio za kutwaa taji hilo.



.png)
0 comments:
Post a Comment