Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geoffrey Nyange ''Kaburu' akiwa na Okwi Uwanja wa ndege jana Kaburu ataondoka kesho.
Nahodha wa Simba, Juma Kaseja akihojiwa na Waandishi wa Habari Uwanja wa ndege jana.
Kaburu akizungumza na Kaseja
Wachezaji wa Simba wakiingia ndani Uwanja wa ndege tayari kwa safari
TIMU ya soka ya Simba imefika salama usiku wa jana mjini
Khartoum Sudan, tayari kwa mchezo wa mwisho mwa wiki wa marudiano, hatua ya 16
Bora Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Simba liyoondoka Dar es Salaam jana alasir,
inahitaji sare tu kwenye mchezo huo kusonga mbele, baada ya kushinda 3-0 katika
mchezo wa kwanza Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa timu hiyo, Milovan Cirkovic
alisema jana wakati timu hiyo ikiondoka kwamba kama vijana wake wakicheza
vizuri hana hofu kwamba watawang’oa Wasudani na kusisitiza kuwa maandalizi yao
wapo vizuri.
Simba ndiyo wawakilishi pekee wa Tanzania
waliobaki katika michuano inayoandaliwa na CAF kwa ngazi ya klabu, ambapo
wawakilishi wengine wa Tanzania ambao tayari wameshatolewa ni Yanga iliyotolewa
na Zamalek ya Misri katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Mafunzo
iliyokuwa ikicheza Ligi ya Mabingwa Afrika na kutupwa nje na Maqulmano ya
Msumbiji.
Nayo Jamhuri ya Pemba ilitolewa michuano ya
Kombe la Shirikisho na Hwangwe FC ya Zimbabwe.
Katika hatua hiyo inayofuata kama Simba
itafuzu, itacheza na moja kati ya timu nane zitakazotolewa raundi ya pili ya
Ligi ya Mabingwa Afrika na ikivuka hapo itaingia hatua ya makundi
itakayohusisha timu nane zitakazokuwa kwenye makundi mawili tofauti.
Simba imekwenda huko na wachezaji 19 na
viongozi saba ambao ni Juma Kaseja, Ally Mustafa,
Shomari Kapombe, Derick Walulya, Amir
Maftah, Juma Jabu, Obadia Mungusa, Kelvin Yondani, Victor Costa, Jonas Mkude,
Mwinyi Kazimoto, Patrick Mafisango na Uhuru Selemani.
Wengine ni Haruna Moshi, Machaku Salum,
Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Edward Shija na Gervais Arnold Kago, wakati viongozi
ni Mwenyekiti Alhaj Ismail Aden Rage, Swedy Nkwabi, Cirkovic, Kocha Msaidizi
Amatre Richard, kocha wa makipa James Kisaka, daktari Cosmas Kapinga, Meneja Nicholaus
Nyagawa na Kamwaga.
Mkuu wa msafara ni Mjumbe wa Kamati ya
Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Hussein Mwamba.






.png)
0 comments:
Post a Comment