| Nchunga kulia |
MWENYEKITI wa Yanga, Wakili Lloyd Baharagu
Nchunga amesema hatajizulu na hawajibiki kwa wazee wachache wanaompiga fitina,
bali wanachama.
Gazeti la Mwananchi leo limeandika kwamba
uongozi wa Yanga ukipuuza shinikizo zito la kutakiwa kujiuzulu toka baadhi ya
wanachama wa klabu hiyo kwa madai ya kuwa kiini cha kipigo cha aibu toka Simba
Jumapili iliyopita, wachezaji tisa timu hiyo wamekalia kuti kavu baada ya
mikataba yao kufikia.
Wachezaji hao wako hatarini kutemwa kwa
sababu kuna uwezekano mdogo, au usiwapo kabisa kusaini mikataba mipya, taarifa
za ndani toka klabu hiyo ya Jangwani zimedai
Ni pamoja na Shamte Ally, Jerry Tegete,
Chacha Marwa, Mohamed Mbegu, Abuu Ubwa, Zuberi Ubwa, Kigi Makasi, Shadrack Nsajigwa na Athuman Idd
'Chuji'.
Tegete anahusishwa kwenda Simba, wakati
Nsajigwa anatuhumiwa kucheza chini ya kiwango katika mechi yao dhidi ya Simba,
ambapo alisababisha penalti mbili kati ya tatu na kuwapa mahasimu wao ushindi
wa mabao 5-0.
"Wachezaji wengi wamemaliza mikataba
yao, wapo baadhi huenda wakaongezewa kama Chuji, lakini wengine watatemwa
akiwamo Shamte ambaye hakuna ubishi hatarudi Jangwani msimu ujao," alisema
mtoa habari.
Alisema wachezaji Nurdin Bakari, Hamis
Kiiza, Kenneth Asamoah bado wana mkataba wa mwaka mmoja, wakati Yaw Berko na
Davis Mwape mikataba yao itamalizika Novemba mwaka huu.
"Uongozi umeshaanza kuzungumza na
Berko kuangalia uwezekano wa kuongeza mkataba wake, lakini Mwape hatacheza
Yanga msimu ujao mara baada ya mkataba wake kumalizika," alisema mpashaji
huyo habari.
Jumamosi wiki hii Kamati ya Utendaji
itakutana, na moja ya mambo watakayozungumza ni ushiriki wa Ligi Kuu,
changamoto zilizokuwepo na kujadili wachezaji watakaochwa na wanaostahili
kubaki.
"Kikubwa kinachoangaliwa ni nidhamu wa
wachezaji ndani na nje ya uwanja pamoja na kiwango, na pia kuna wachezaji
wengine watahama kwenda timu nyingine haya yote yataangaliwa."
Alisema ajenda nyingine kwenye kikao hicho
ni kupanga tarehe ya Mkutano Mkuu wa wanachama pamoja na vuguvugu la mgogoro
lililopo ndani ya klabu hiyo.
Mwenyekiti wa Yanga Llody Nchunga alisema
masuala yote yanayohusu usajili wa wachezaji watawekwa wazi wiki ijayo mara
baada ya kikao chao cha Kamati ya Utendaji.
Aidha, kuhusu wachezaji wanaodai, Nchunga
alisema ni wale waliongezewa mikataba ambao ni Nurdin Bakari na Nadir Haroub.
"Wachezaji wanaodai fedha za usajili
ni wachache tena waliongezewa mikataba kipindi cha uongozi uliopita na hata
hivyo fedha hizo wanatakiwa walipwe msimu ujao kwa kuwa ndiyo watakaoanza
kuutumikia," alisema Nchunga na kuwataja wachezaji hao kuwa ni Nurdin na
Nadir.
"Nawashangaa wazee wetu wanavyosema
wachezaji wanadai Sh127 milioni. Hivi hawa wazee ni wahasibu? Wamepata wapi
hesabu hizi, napenda kuwaambia kuwa hatudaiwi kiasi hicho," alisema.
Kuhusu shinikizo la kutakiwa kujiuzulu,
Nchunga alisema hawezi kufanya hivyo kwa shinikizo la watu wachache wakati
Yanga ni timu ya wanachama.
"Mimi nilichaguliwa na wananchana wa
Yanga, wao ndiyo wanaweza kunitaka nijiuzulu tena kupitia Mkutano Mkuu wa
Klabu. Tunaendeshwa na katiba na siyo kelele za vikundi vya watu. Hatima yangu
itaamuliwa na Wanayanga, siyo kikundi.
"Kamati ya Utendaji itapanga tarehe ya
Mkutano Mkuu, mimi nafuata katiba na wala sing'ang'anii madaraka Yanga. Wale
wote wanaotaka mimi na uongozi wangu tujiuzulu, basi waje kwenye mkutano
mkuu," alisema bosi huyo.
Alisema utamaduni wa kuondoa madarakani
uongozi kwa njia za mkato umepitwa na wakati. "Mambo ya kupinduana
yamepitwa na wakati, dhambi hii ya kupinduana haitaishia kwa Nchunga peke yake
itawatafuta wengine. Ifike mahali tubadilike tufanye kazi kwa kufuata katiba na
siyo mazoea."
Aliongeza: "Wanaona sifai wafuate
taratibu na watoe sababu za msingi siyo kwa vile tumepokwa pointi tatu ndiypo
wanishinikize nijiuzulu hayo ni makosa ya soka.
Naomba itoshe kusema hivi...wale wote
wanaodhani nitajiuzulu nafasi yangu, ni wazi wamepitwa na wakati. Sijiuzulu kwa
sababu ya kikundi cha watu wachache, wanachama ndiyo wataamua."
Kuhusu madai ya kocha wa Yanga Kostadin
Papic, Nchunga alisema: "Papic tunamuandalia malipo yake ambayo ni
mishahara ya miezi miwili na muda wowote atalipwa.
Alikiri uongozi wake kutokuwa na
ushirikiano na Papic kwa sababu kocha mwenyewe amekuwa akionyesha dharau mbele
ya uongozi kwa kushindwa kuheshimu maagizo anayopewa.
"Sikiliza nikuambie, Papic hatuwezi
kuwa naye tena tunamuandalia chake aondoke, kwanza hata wachezaji hawamtaki.
Tulishawahi kumuonya kuhusu kutoa mambo ya ndani ya klabu kwenye vyombo vya
habari lakini hakuwahi kutekeleza agizo hilo.
"Mechi ya Toto kule Mwanza alichangia
kwa kiasi kikubwa tukapoteza mchezo. Kwanza alikataa kwenda na timu, baadaye
akataka atumiwe tiketi aende Mwanza akatumiwa kufika tu wachezaji wakakosa
raha.
Hata hivyo Nchunga hakutaka kuweka wazi
mbadala wa Papic kwa madai kuwa Kamati ya Utendaji ndiyo itakayoamua hatima
yake. Hata hivyo kuna taarifa klabu hiyo ipo kwenye mchakato wa kupitia
vielelezo vya makocha kutoka Romania na Scotland.


.png)
0 comments:
Post a Comment