• HABARI MPYA

    Sunday, May 13, 2012

    SAMATTA, MAZEMBE WATINGA NANE BORA AFRIKA


    Sixième quart consécutif pour Mazembe !
    Sinkala



    TOUT Puissant Mazembe imefuzu kuingia Nane Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kwa mara ya sita mfululizo baada ya kutoa sare ya 1-1 na wenyeji El Merreikh kwenye Uwanja wa Omdurman, Khartoum jana, Mazembe, yenye mshambuliaji mwingine Mtanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu, lakini ‘anasugua mwanzo mwsiho’, ilitangulia kupata bao kupitia kwa Nathan Sinkala.
    Mazembe imefuzu kwa ushindi wa jumla wa 3-1, baada ya awali kushinda 2-0 nyumbani, Mbwana Ally Samatta wa Tanzania akifunga bao moja.
    Merreikh ilisawazisha kupitia kwa mchezaji wake Mganda, Mike MUTYABA dakika ya 61.
    Kama kawaida, mshambuliajio chipukizi wa Tanzania, Mbwana Ally samatta alikuwa mwiba mchungu kwenye safu ya ulinzi ya Merreikh na hata bao la jana lina mchango wake.
    Sasa ni wakati wa Samatta kujiuza zaidi kupitia mechi sita atakazocheza kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa- na kutokana na ndoto za Mazembe kuchukua ubingwa, kuna uwezekano kinda huyo wa Tanzania mwishoni mwa mwaka akaweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza Klabu  Bingwa ya Dunia ya FIFA. 


    GONGA CHINI KILA PICHA UIONE KWA UKUBWA HALISI Al Merreikh  Vs TP Mazembe

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA, MAZEMBE WATINGA NANE BORA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top