![]() |
Kikosi cha Simba |
WEKUNDU wa Msimbazi, Simba SC leo wana kazi moja tu ya kumalizia kazi waliyoifanya kwa kiasi kikubwa Dar es Salaam, wiki mbili zilizopita.
Simba leo itakuwa uwanjani Sudan kumenyana
na Al Ahly Shendi ya huko katika mechi ya pili ya raundi ya tatu ya michuano ya Kombe
la Shirikisho.
Simba iliondoka jijini Jumanne kuelekea
Sudan kwa ajili ya mechi hiyo ambapo hata hivyo hawakupata mapokezi mazuri
kutoka kwa wenyeji wao hali ilioufanya uongozi wa klabu
hiyo kuazimia kupeleka malalamiko (CAF).
Simba leo inahitaji ushindi au kama
kufungwa isiwe zaidi ya mabao 3-0 ili isonge mbele hatua inayofuata ya michuano
hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika mechi ya kwanza
iliyochezwa wiki mbili zilizopita kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Habari kutoka Sudan zinasema pamoja na
vituko walivyofanyiwa na wenyeji, lakini kikosi cha Simba kiko imara kwa ajili
ya mechi hiyo itakayochezwa katika mji wa Shendi.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba Ezekiel
Kamwaga Simba imefanyiwa vitendo ambavyo si vya kiuanamichezo ikiwa ni pamoja
na kusafirishwa umbali mrefu, kupewa chakula usiku sana pamoja na kulazwa
kwenye hosteli badala ya hoteli nzuri kama walivyofanyiwa wao
walipofika nchini.
Kamwaga alisema wachezaji wako kwenye hali
nzuri na kocha Milovan Circovick ameahidi kuibuka na ushindi.
“Kila kitu chetu kwa upande wa benchi la
ufundi kiko sawa, pamoja na vurugu zao lakini tunaamini dakika 90 uwanjani ndio
zitaongea,” alisema Kamwaga.
“Wachezaji wako kwenye ari kubwa pamoja na
mizengwe ya hapa na pale, kwani hawakukatishwa tamaa badala yake walifanya
mazoezi wenyewe pamoja na kocha kuwapa
mapumziko… wachezaji wanasema lengo lao ni
kuvuka raundi inayofuata na watavuka hata wakiwafanyiwa vituko,”alisema
Kamwaga.
Mungu ibariki Simba. Ibariki Tanzania. Amiiin.
VIKOSI VYA LEO:
SIMBA SC:
Kikosi cha Simba leo kinatarajiwa kuwa; Juma
Kaseja. Shomari Kapombe, Amir Maftah, Victor Costa, Kelvin Yondan, Mwinyi
Kazimoto, Uhuru Suleiman, Patrick Mafisango, Felix Sunzu, Haruna Moshi na Emmanuel
Okwi, wakati kwenye benchi watakuwapo Ally Mustafa
‘Barthez’, Obadia Mungusa, Juma Jabu, Derrick
Walullya na Salum Machaku.
Al AHYL SHANDY:
Abdulrahma Ali, Elnour Altigani, Isaac Seun
Malik, Saddam Abu Talib, Fareed Mohamed/Orwah Ibrahim dk 83, Zakaria Nasu,
Razak Yakubu, Faris Abdallah, Hamopuda Bashir/Mogabid Farouq dk63, Nadir
Eltaveb na Bashiro Ubamba.
Mungu ibariki Simba. Ibariki Tanzania. Amiiin.
0 comments:
Post a Comment