• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    TBL KUIDHAMINI TAIFA STARS KWA BILIONI 23

    Tenga wa pili kutoka kushoto na Robin anayemfuatia wakisaini mkataba. pembeni yao ni mawakili wao. na nyuma kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, Makamu wa kwanza wa rais wa TFF, Athumani Nyamlani, Meneja wa Kilimanjaro, George Kavishe, Mkurugenzi wa Michezo, Leonard Thadeo, Meneja Masoko wa TBL, Jimmy Kabwe na Ofisa wa Wizara, Juliana Yassoda. 
    Tenga na Robin wakipeana mikono na kubadilishana makabrasha baada ya kusaini mkataba

    Burudani ya mabinti


    Tenga na Mgongolwa wakifurahia

    Tenga na Mgongolwa

    Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah kushoto, katikati mama Juliana Yassoda na kulia Robin

    Wadau wa soka, Msafiri Mgoyi Mjumbe wa TFF, beki wa zamani Taifa Stars na Meneja wa timu hiyo, Leopold Mukebezi, Fred na kocha Joseph Kanakamfumu

    Mwandishi wa Nipashe Somoe Ng'itu na kocha Jamhuri Kihwelo

    Makamu wa kwanza wa rais wa TFF, Athumani Nyamlani na Mdau Salim

    KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), jioni hii imeingia mkataba wa kuidhamini timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wa miaka mitano, wenye thamani ya Sh. Bilioni 23.
    Uzinduzi huo ulifanyika katika hoteli ya Kempinski, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wote wakuu wa TFF, TBL na wadau mbalimbali.
    Stars, ambayo tangu mwaka 2006, ilikuwa ikidhaminiwa na kampuni nyingine ya Bia Tanzania, Serengeti (SBL) sasa itakuwa ikivaa jezi zenye nembo ya bia ya Kilimanjaro, ambayo pia ni wadhamini wa Simba na Yanga.
    Rais wa TFF, Leodegar Chillah Tenga alitiliana saini mkataba huo na Mkurugenzi Mkuu wa TBL, Robin Goetzsche katika hafla iliyopambwa na burudani nyepesi nyepesi.
    Katika hafla hiyo liyofana, utiaji saini wa mkataba huo, ulishuhudiwa na mawakili wa pande zote mbili, TFF ikiwakilishwa na Alex Mgongolwa.
    Kwa mujibu wa maridhiano hayo, TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager itaidhamini Taifa Stars kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo.
    Hii ni mara ya kwanza kwa kampuni hiyo kubwa ya bia kutoa udhamini kwa timu ya taifa, hata hivyo huko nyumba TBL iliwahi kushiriki katika udhamini wa masuala ya soka kwa miaka minne nyuma huku ikidhamini Taifa Cup na vilabu vikubwa vya Simba na Yanga.
    Akizungumza katika hafla hiyo ya kutiliana saini, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL, Robin Goetzsche alisema udhamini huoi utafungua mwanga mpya katika medani ya soka nchini Tanzania.
    “Tunasaini mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya dola za Marekani milioni 10 na katika kipindi chote hicho kaulimbiu yetu itakuwa “Fikisha Soka ya Tanzania Katika Kilele cha Mafanikio” na kutupa kila sababu ya kujivunia kilicho chetu
    Tuna matarajio makubwa sana na timu ya taifa kwani tunaamini kuwa ina uwezo wa kufanya maajabu, na kama nilivyosema awali, hili ni pambazuko la kuelekea mafanikio. Uwekezaji wetu umelenga katika kuhakikisha kambi za mazoezi zinaimarishwa, wachezaji watalala katika hoteli zenye ubora wa juu zenye zaidi ya ngazi tatu zilizo na bwawa la kuogelea na vifaa vya mazoezi, vifaa vinaboreshwa na pia vijana watapata fursa za kucheza mechi nyingi za kirafiki ili wajipime nguvu na kupata uzoefu zaidi na timu zinapata basi jipya la kisasa.
    Kwa kuongeza, alisema udhamini wao utasaidia katikau nunuzi wa vifaa mbalimbali vya kisasa vya michezo, mafunzo kwa wafanyakazi wa TFF ndani na nje ya nchi, uendeshaji wa tovuti ya TFF, Semina na mikutano ya utawala bora.
    Wakati huo huo, TBL kupitia bidhaa yake nyingine, Grand Malt, ambacho ni kinywaji kisicho na kilevi itakuwa kikidhamini Ligi Kuu ya Zanzibar. Hii ni kuonyesha namna TBL ilivyo mstari wa mbele katika kuhamasisha soka si kwa Bara tu bali na Visiwani. Mkataba huu ni wa miaka mitatu na utamalizika mwaka 2015 ukiwa na thamani ya Sh milioni 140 kila mwaka.
    Kwa upande wake, Rais wa TFF, Lodger Tenga aliahidi kutoa ushirikiano thabiti kwa wadhamini wapya kwani anaamini mkataba huo utaleta mapinduzi chanya katika soka nchini Tanzania. Hata hivyo, aliwaomba Watanzania kuwa na uzalendo kwa timu yao ya taifa kwa kuishangilia kwa wingi kwenye mechi zake.
     “Hakuna jema lolote kama tutakuwa na ari ya kuzishabikia timu za nje badala ya ya timu ya nyumbani, wachezaji wetu wanahitaji moyo wawapo uwanjani kwa kushangiliwa ipasavyo,” alisema.
    Naye Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema udhamini huo ni wa thamani na kwamba watafanya kila liwezekanalo kuisaidia TFF kuhakikisha kuwa Taifa Stars inang’ara katika anga za kimataifa na hivyo kukidhi kiu ya Watanzania.
    “Hii ni mara ya kwanza kuidhamini Taifa Stars na tunataka kuja kwa mtindo mpya na wa kipekee, tunataka Watanzania wajivunie timu yao kwa
    sababu ukarimu huanzia nyumbani…tuwape moyo wachezaji wetu na tujivunie kilicho chetu,” alisema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TBL KUIDHAMINI TAIFA STARS KWA BILIONI 23 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top