• HABARI MPYA

    Wednesday, May 09, 2012

    DROO YA PILI VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO YAFANYIKA LEO

    Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Teddy Mapunda akizungumza na Waandishi wa Habari leo asubuhi katika kwenye chumba cha mikutano cha SBL, Oysterbay, Dar es Salaam kuhusu promosheni ya VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO.

    DROO ya pili ya  Promosheni inayoendelea ya kampuni ya bia ya Serengeti inayojulikana kama‘Vumbua hazina chini ya kizibo’ imefanyika leo katika ofisi za kampuni hiyo maeneo ya Oysterbay jijini Dar Es salaam.
    Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Teddy Mapunda amesema leo asubuhi katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake, Oysterbay, Dar es Salaam kwamba kupitia bidhaa zao, Serengeti Premium Lager, Tusker Lager na Pilsner Lager inaendesha promosheni nchi nzima ijulikanayo kama “ VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO.’
    Teddy ‘Smart Lady’ alisema Promosheni hii ya aina yake iliyosheheni zawadi mbalimbali kubwa na ndogo kama vile Jenereta (kangavuke), Pikipiki, Bajaji, Gari ndogo aina (saloon) na zawadi zingine nyingi zikiwemo pesa taslimu. Katika promosheni hii zawadi za thamani zaidi ya Tsh MILLIONI 780 kushindaniwa.
    “Droo hiyo ilihudhuriwa na waandishi wa habari, wasimamizi kutoka Bodi ya Bahati Nasibu Tanzania, wadau kutoka ndani na nje ya kampuni hiyo, wakiwemo kampuni ya kuendesha Bahati Nasibu ya PUSH MOBILE, wahakiki na wakaguzi kutoka PWC-Price Water House Coopers ili kuhakikisha washindi wote wanapatikana kihalali,”alisema.
    “Tayari tuna washindi zaidi ya elfu moja mia tano, wamejishindia pesa taslimu na kuzipata kupitia njia ya MPESA.  Hawa washindi ni pamoja na wanaoshinda bidhaa zenyewe zilizoorodheshwa katika promosheni hii.  Vile vile,  kama mlivyoshuhudia asubuhi ya leo, tumepata washindi wawili wa jenerata, na sio mmoja kama ilivyo kawaida .  Hii ni kwa sababu katika promosheni hii, kuna vigezo na masharti yanayozingatiwa” aliongeza.
    Alisema masharti ya promosheni hii wanayazingatia, kwa sababu hiyo, mshindi wa wiki iliyopita wa jenerata ilikuja kugundulika hakustahili kushiriki katika promosheni hii. 
    “Tunataka kuwaeleza watanzania  kwamba hii promosheni ni ya uhakika na kwa kweli mnavyoona, ina uangalizi mkubwa na inaendeshwa kwa umakini kabisa.  Nawaomba wateja wetu waendelee kushiriki ili waendelee kushinda.” Aliongeza mkurugenzi huyo.
    Washindi  katika droo ya leo waliojishindia jenereta ni Amadeus Minja mkazi wa pugu na Agnes Msengi wote wakia ni wakazi wa jijini Dar Es Salaam na Ibrahim Kimambo mkazi wa Tabata Kimanga jijini Dar Es Salaam aliyejishindia Pikipiki .   Allan Peter Chonjo, Meneja wa Bia ya Serengeti Premium Lager alipiga simu kwa washindi na ilikuwa dhahiri kwamba washindi walishtuka na kufurahia ushindi wao.  Baada ya maongezi machache yaliyofanyika kwa njia ya simu washindi hao waliweza kujieleza vizuri majina yao kamili na wanapopatikana ili waweze kupatikana siku chache zijazo kwenye hafla fupi ya kuwakabidhi zawadi zao.

    MAELEKEZO:
    Nunua bia ya Serengeti Premium Lager, Tusker Lager au Pilsner Lager fungua kisha angalia ndani ya kizibo  utapata namba saba zilizochanganyika na herufi.
    Fungua sehemu ya kutuma ujumbe mfupi kwenye simu yako, nakili namba na herufi hizo mfano TS5555P, na uzitume kwenda 15317 na utapokea ujumbe mfupi wa maneno ambao utasema kama umejishindia pesa taslimu kati ya shilingi 10,000 au 50,000 au 100,000 ambayo itatumwa kwako kwa njia ya MPESA. Au unaweza kupata ujumbe utakao kwambia kuwa namba yako imeingia kwenye droo ya bahati nasibu na utaweza kujishindia zawadi kubwa kama vile jenereta, gari ndogo , bajaji au pikipiki
    Katika promosheni hii pia unaweza kujipatia bia ya bure papo hapo kila utakapoona alama ya chupa ndani ya kizibo na unaweza kupata kati ya bia tatu zilizoainishwa katika promosheni hii.  Pia unaweza kupata maelekezo katika vipeperushi na magazeti.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DROO YA PILI VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO YAFANYIKA LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top