• HABARI MPYA

    Friday, September 07, 2012

    BEKI YANGA AOMBEWA ITC KUCHEZA URENO

    Abuu Ubwa

    Na Prince Akbar
    BEKI aliyetupiwa virago katika klabu baada ya msimu uliopita, Abuu Zuberi Ubwa mwenye umri wa miaka 20, ameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) na Shirikisho la Soka Ureno (FPF) ili acheze soka ya kulipwa huko.
    Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, mbali na Ubwa, beki wa kushoto ambaye alishindwa kung’ara Yanga, kwa misimu miwili ya kuwa na klabu hiyo, Hamisi Thabit Mohamed mwenye umri wa miaka 19, pia kutoka African Lyon pia ameombewa ITC ya kucheza nchi hiyo.
    Kwa mujibu wa FPF, wote wawili wanaoombewa ITC kama wachezaji wa ridhaa (amateur) ili waweze kujiunga na timu ya Atletico Sport Clube ya Ureno ambayo hata hivyo haikuelezwa iko daraja gani nchini humo.
    Pia FPF imeombwa kupatiwa hati ya maelezo ya mchezaji (player’s passport) kwa kila mmoja ikiwemo taarifa za ushiriki wao katika mechi rasmi zinazotambuliwa na TFF wakiwa katika klabu zao hizo za zamani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BEKI YANGA AOMBEWA ITC KUCHEZA URENO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top