• HABARI MPYA

    Thursday, September 06, 2012

    HANS POPPE AMCHANGIA DOLA 1,000 MODEST


     Zakaria Hans Pope
    Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope (kushoto) akimkabidhi mchango wa dola 1,000 Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Said Kilumbanga kwa ajili ya kusaidia matibabu ya mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa Stars, Alfonce Modest. Modest kwa nyakati tofauti aliwahi kuzichezea timu za Simba, Mtibwa Sugar, Pamba, pamoja na Mlandege ya Zanzibar. Picha kwa hisani ya Habari Mseto Blog.
    Na Mwandishi Wetu
    MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ametoa msaada wa dola za Kimarekani 1,000 (zaidi ya Sh milioni 1.5) kwa beki wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Alphonce Modest Pambamotosapi, anayesumbuliwa na maradhi ya ganzi.
    Modest, aliyewahi kuchezea Pamba ya Mwanza, Simba, Yanga za Dar es Salaam, Mlandege ya Zanzibar na Mtibwa Sugar ya Morogoro, yuko Dar es Salaam akiendelea na matatibu chini ya usimamizi wa gazeti la Championi kwa kushirikiana na Redio ya Magic FM.
    Mtangazaji wa Magic FM, Said Kilumanga ambaye ni mmoja wa waratibu wa zoezi hilo alisema tayari Hans Poppe ameshakabidhi fedha hizo, ili kumsaidia beki huyo wa kushoto, aliyempokea Kenneth Mkapa katika nafasi hiyo timu ya taifa.
    “Tunamshukuru sana Hans Poppe kwa moyo wa kujitolea, wengine pia wajitokeze kumsaidia kwa kuwa amepungukiwa kama Sh 600,000 tu ili kukamilisha matibabu yake,” alisema Kilumanga.
    Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama ndiye alikuwa mdau wa kwanza kumchangia Modest na kuomba wengine wajitokeze kumsaidia beki huyo mahiri wa zamani.
    Baadhi ya wanamichezo wamekuwa wakiendelea kumchangia Modest ili kuhakikisha anapata matibabu baada ya maradhi hayo kumuandama kwa zaidi ya miaka minne sasa.
     (Wanaotaka kumsaidia Modest, wanaweza kupiga namba 0718 427426  na 0718 427426 kufikisha misaada yao).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HANS POPPE AMCHANGIA DOLA 1,000 MODEST Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top