• HABARI MPYA

    Monday, April 08, 2013

    HANS POPPE ASEMA HARUDI SIMBA SC HADI KWANZA RAGE AMALIZANE NA WABAYA WAKE AMANI IREJEE KLABUNI


    Na Mahmoud Zubeiry
    HIVI karibuni, Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj  Ismail Aden Rage pamoja na kusema ataitisha Mkutano Mkuu wa mwaka Julai mwaka huu, pia alisema amekubali kujiuzulu kwa Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ na si Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Zacharia Hans Poppe, aliyekuwa pia Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili. 
    Rage, alisema ataongoza mwenyewe kampeni za kuhakikisha Hans Poppe anabatilisha uamuzi wake wa kujiuzulu na kuendelea kuitumikia Simba SC. Je, nini msimamo wa Hans Poppe juu ya hili? Fuatilia mahojiano haya baia ya BIN ZUBEIRY na Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
    Hans Poppe; Siriui hadi Rage akae na wabaya wake wamalizane amani irudi

    BIN ZUBEIRY: Habari za leo kiongozi
    HANS POPPE: Nzuri tu, habari na wewe
    BIN ZUBEIRY: Salama, Hivi mlizungumza na Rage kuhusu suala la wewe kubatilisha uamuzi wako wa kujiuzulu?
    HANS POPPE: Hapana, bado
    BIN ZUBEIRY: Nani anakwamisha mazungumzo kati yenu?
    HANS POPPE: Nafasi tu, mimi nimetingwa sana, tangu Pasaka sijatulia Dar es Salaam, hadi nitakapotulia
    BIN ZUBEIRY: Wewe ndiye unakwamisha kwa hivyo…lakini kwa kuwa somo unalijua, mtazamo wako ukoje?
    HANS POPPE: Nimewashauri wakae kwanza, warejeshe amani, vinginevyo ni kazi bure
    BIN ZUBEIRY: Labda wanaamini wewe ukirudi, utasaidia kurejesha amani, unaonaje?
    HANS POPPE: Sitarudi hadi kwanza (Rage) azungumze na wanaompinga
    BIN ZUBEIRY: Kama msimamo wa Rage uko tofauti na wazo lako, nini mustakabali wa klabu hapa? 
    HANS POPPE: Lazima wakubali kukutana kwa maslahi ya klabu
    BIN ZUBEIRY: Hakuna njia nyingine ya kuinusuru klabu dhidi ya misimamo ya Mwenyekiti? 
    HANS POPPE: Hakuna
    BIN ZUBEIRY: Wana Simba wana imani na wewe na wanakutegemea, kushikilia msimamo wako kwa upande mwingine huoni kama unawaangusha? 
    HANS POPPE: Siwezi kusaidia kama hakuna amani, kwa hivyo nikiwakutanisha wakaelewana, hakutakuwa na taabu. Shida ni Rage na mdomo wake.
    BIN ZUBEIRY: Namini wewe ni Simba damu…
    HANS POPPE: Haswaa
    BIN ZUBEIRY: Unajisikiaje timu yako inafanya vibaya, kocha hajapata mishahara miezi miwili, klabu inakabiliwa na madeni lukuki, wachezaji hawana ari…vurugu tupu…
    HANS POPPE: Inasikitisha na wengi wananipigia, lakini hiyo ndio faida ya ugomvi
    BIN ZUBEIRY: Mtakuwa tayari kuvumilia hadi Rage amalize muda wake madarakani?
    HANS POPPE: Mimi sina upande, lazima atambue kama hatazungumza nao, hali haitabadilika, kwa hivyo yeye ameshika dhamana ya Simba SC
    BIN ZUBEIRY: Lakini unashindwaje kummudu Rage na ni rafiki yako sana, ambaye mnashirikiana hadi katika mambo binafsi?
    HANS POPPE: Amekubali kukutana, tatizo utekelezaji
    BIN ZUBEIRY: Alikupa ahadi hiyo wewe?
    HANS POPPE: Ndiyo, nilimshauri hivyo na akakubali. Inatosha bwana, naingia kwenye mkutano sasa. 
    BIN ZUBEIRY: Asante kiongozi, kazi njema.
    HANS POPPE: Asante nawe na karibu tena.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: HANS POPPE ASEMA HARUDI SIMBA SC HADI KWANZA RAGE AMALIZANE NA WABAYA WAKE AMANI IREJEE KLABUNI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top