• HABARI MPYA

    Saturday, April 13, 2013

    MESSI NA INIESTA WATEMWA BARCA KIKOSI KITAKACHOIVAA ZARAGOZA KESHO



    Lionel Messi 


    KLABU ya Barcelona imemtema Mwanasoka Bora wa Dunia, Lionel Messi wachezaji wa kimataifa wa Hispania, Andres Iniesta, Sergio Busquets na Jordi Alba katika kikosi kitakachoivaa Zaragoza kesho.
    Messi alicheza nusu ya mwisho ya kipindi cha Jumatano katika Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris Saint-Germain licha ya kuwa anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja na hakutarajiwa kucheza hadi mechi ya kwanza ya Nusu Fainali  dhidi ya Bayern Munich, Aprili 23.
    Busquets pia ameenguliwa kwenye kikosi hicho kwa sababu ya kuwa majeruhi, wakati Iniesta na Alba kuondolewa kwao ni maamuzi ya menejimenti.
    Habari njema kwa Azulgrana ilikuwa ni kurejea mazoezini kwa Adriano leo na ameingizwa kwenye kikosi cha wachezaji 18 kinachokwenda Zaragoza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MESSI NA INIESTA WATEMWA BARCA KIKOSI KITAKACHOIVAA ZARAGOZA KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top