• HABARI MPYA

    Sunday, April 14, 2013

    VAN PERSIE AMALIZA GUNDU MAN UNITED IKIUA 2-0, VURUGU ZATAWALA PAMBANO LA NEWCASTLE NA SUNDERLAND



    MSHAMBULIAJI Robin van Persie amemaliza ukame wa mabao Manchester United akiiwezesha timu hiyo kupaa kileleni mwa Ligi Kuu kwa pointi 15 zaidi baada ya kuilaza Stoke City mabao 2-0.
    Van Persie alikuwa amecheza mechi 10 za mashindano ya nyumbani bila kufunga, lakini leo amefunga bao la pili kwa penalti dakika ya 66, baada ya
    Michael Carrick kufunga la kwanza dakika ya nne na sasa United inahitaji pointi saba tu katika mechi zake sita zilizobaki ili kuivua ubingwa Manchester City.
    Katika mchezo wa leo vikosi vilikuwa; Stoke: Begovic, Cameron/Jerome dk71, Huth, Shawcross, Wilkinson, Shotton, Whelan, Nzonzi, Adam, Jones/Crouch dk84 na Walters/Owen dk77.
    Manchester United: De Gea, Evra, Jones, Ferdinand, Vidic, Valencia, Carrick, Kagawa, Rooney, Hernandez/Welbeck dk77 na Van Persie.

    One step closer: Goalscorers Michael Carrick and Robin van Persie congratulate eachother on United's victory
    Pati la ushindi: Wafungaji wa mabao ya United, Michael Carrick na Robin van Persie wakipongezwa na wenzao
    Tony Pulis
    Sir Alex Ferguson
    Makocha: Tony Pulis kushoto wa Stoke na Sir Alex Ferguson kulai wa United leo

    Katika mchezo mwingine, Sunderland iliichapa Newcastle mabao 3-0, lakini mashabiki 27 walikamtwa na Polisi watatu walijeruhiwa kufuatia vurugu zilizoibuka uwanjani.
    Vurugu zilitokana na kundi la mashabiki wa Newcastle kujaribu kuwavamia mashabiki wa Sunderland baada ya kipigo Uwanja wa nyumbani, St James' Park.
    Dragged away: Newcastle fans were involved in fights with police following their side's derby defeat
    Safari lupango: Shabiki wa Newcastle akisongeshwa na Polisi
    Dragged away: Newcastle fans were involved in fights with police following their side's derby defeat
    Dragged away: Newcastle fans were involved in fights with police following their side's derby defeat

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: VAN PERSIE AMALIZA GUNDU MAN UNITED IKIUA 2-0, VURUGU ZATAWALA PAMBANO LA NEWCASTLE NA SUNDERLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top