• HABARI MPYA

    Saturday, April 13, 2013

    YANGA ILIVYOIVUA UBINGWA RASMI SIMBA SC LEO TAIFA

    Mshambuliaji wa Yanga SC, Didier Kavumbangu akiwatoka mabeki wa JKT Oljoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 3-0.

    Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima (kushoto) akimtoka kiungo wa JKT Oljoro, mbele ya refa Amon Paul

    Mtaalamu; Haruna Niyonzima akijiandaa kupiga kona

    Didier Kavumbangu akigombea mpira na beki wa JKT Oljoro

    Hamisi Kiiza wa Yanga katikati akimtoka beki wa Oljoro kulia. Kushoto ni mshika kibendera namba moja, John Kanyenye akifuatilia mwenendo

    Frank Domayo kulia akipenyeza mpira pembeni ya kiungo wa Oljoro, Hamis Saleh

    Didier Kavumbangu akigombea mpira na beki wa Oljoro 

    Didier Kavumbangu akiwania mpira wa juu dhidi ya beki wa JKT Oljoro nyuma yake

    Didier Kavumbangu akiwa amemuangukia kipa wa JKT Oljoro, Mussa Lucheke huku beki Nurdin Mohamed akiondoka na mpira

    Sekeseke; Beki wa Oljoro akiwa hewani kupiga mpira wa kichwa wakati wa kizazaa langoni mwao

    Hamisi Kiiza akikosa bao baada ya kipa Mussa Lucheke kuokoa mpira ambao hata hivyo ulimponyoka...

    Hamisi Kiiza akijaribu kumpokonya mpira kipa wa Oljoro, Mussa Lucheke 

    Raha ya mechi bao; Simon Msuva akishangilia bao lake aliloifungia Yanga leo

    Kipa wa JKT Oljoro, Mussa Lucheke akijaribu kupangua mpira wa juu bila mafanikio. Mpira ulimpita ukaokolewa na beki ukamkuta Nadir Haroub 'Cannavaro' akaukwamisha nyavuni kuipatia Yanga bao la kwanza 

    Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya akimpatia huduma ya kwanza kiungo Athumani Iddi 'Chuji' mbele ya kocha Ernie Brandts kushoto

    Kikosi cha Yanga leo

    Watu wa kazi; Viongozi wa Kamati ya Mashindano ya Yanga SC; Kutoka kulia Abdallah Bin Kleb, Moses Katabaro na Seif Abdallah wakiwa nje ya chumba cha kubadilishia nguo cha wachezaji wao kabla ya mchezo 

    Kikosi cha JKT Oljoro leo

    Simon Msuva akifumua shuti kufunga bao la pili la Yanga

    Said Bahanuzi na Hamisi Kiiza kushoto wakishangilia na Simon Msuva baada ya kufunga  

    Kiungo Athumani Iddi 'Chuji' akiwa ameruka na kipa wa JKT Oljoro, Mussa Lucheke

    Hamisi Kiiza akijiandaa kushangilia bao lake la tatu aliloifungia Yanga SC leo huku Mussa Lucheke akiushuhudia mpira (hauonekani pichani) unavyotinga nyavuni

    Wachezaji wa Yanga Nadir Cannavaro, Haruna Niyonzima na Athumani Iddi wakimlalamikia refa Amon Paul kushoto

    Kocha wa Yanga SC; Ernie Brandts akimpongeza Kiiza. Kulia ni Frank Domayo

    Beki mkongwe wa Yanga SC, Nsajigwa Shadrack akimdhibiti mshambuliaji wa JKT Oljoro

    Said Bahanuzi wa Yanga akifumua shuti pembeni ya Hamisi Kiiza na beki wa JKT Oljoro, Salim Mbonde, Bahanuzi alifunga, lakini refa akasema alikuwa ameotea kabla

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA ILIVYOIVUA UBINGWA RASMI SIMBA SC LEO TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top