IMEWEKWA JULAI 12, 2013 SAA 12:55 ASUBUHI
KIUNGO Victor Wanyama amewatumia ujumbe wa kuwaaga Celtic na mashabiki wao baada ya kukamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 12 kutua Southampton.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Kenya mwenye umri wa miaka 22, ambaye alitambulishwa rasmi St Mary’s baada ya kusaini Mkataba wa miaka minne akipewa mshahara wa Pauni 30,000 kwa wiki, amesema amefurahi mno kutua Ligi Kuu ya Engkand.
Silaha mpya: Mauricio Pochettino akimkaribisha Victor Wanyama kwa Watakatifu
Usajili wake umevunja rekodi ya dau kubwa la usajili la Pauni Milioni 9.5 zilizolipwa na Spartak Moscow kumnunua mchezaji mwingine wa Celtic, Aiden McGeady mwaka 2011. Kwa Southampton imejirudia, kwani kabla ya hapo dau kubwa kwao kutoa kusajili ilikuwa Pauni Milioni 12 walipomnunua mchezaji wa Bologna, Gaston Ramirez msimu uliopita.
Wanyama katika ofisi mpya
Akipambana na walio bora: Wanyama alifunga bao dhidi ya Barcelona msimu uliopita katika Ligi ya Mabingwa
Kujiweka fiti: Wanyama amekuwa mazoezini nchini Ujerumani na mabingwa hao wa Ligi Kuu Scotland