• HABARI MPYA

    Friday, July 12, 2013

    RASMI HIGUAIN AMEOTA MBAWA ARSENAL...PEREZ ASEMA ANABAKI NA JUMATATU ATAKUTANA NAYE FARAGHA

    IMEWEKWA JULAI 12, 2013 SAA 11:36 JIONI
    OMBI la Arsenal kumsajili mshambuliaji, Real Madrid Gonzalo Higuain limekutana na kizingiti kingine baada ya taarifa nchini Hispania kusema kwamba mshambuliaji huyo sasa anajisikia kubaki.
    Kulikuwa kuna taarifa tofauti kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa mika 25 alitarajiwa kuwasili London, kwa ajili ya mipango ya uhamisho wa Pauni Milioni 23 ikifirikiwa makubaliano yalifikiwa wiki mbili zilizopita.
    Rais wa Madrid, Florentino Perez ameyapuuzia madai hayo na gazeti la Marca la Hispania limesema Muargentina huyo atakutana naye Jumatatu kwa mazungumzo.
    Set to stay: The U-turn by Higuain and Real is sure to frustrate Gunners fans
    Anjiandaa kubaki: Kigeugeu cha Higuain na Real hakika kinawachanganya mashabiki wa Gunners

    Timu hiyo ya Hispania inaanza maandalizi ya msimu mpya Jumatatu na sasa inatarajiwa kwamba Higuain atabakia huko, tayari kucheza mechi za mwanzoni za kujiandaa na msimu mpya dhidi ya Bournemouth, Lyon, na Paris Saint-Germain.
    Higuain alionyesha nia yake ya kuondoka Madrid mwishoni mwa msimu uliopita, wakati huo timu ikiwa chini ya Jose Mourinho.
    Lakini sasa inaonekana atakuwa katika mipango ya kocha mpya, Carlo Ancelotti, hususan kutokana na ukweli kwamba hakuna ombi rasmi la kumsajili lililowasilishwa na Arsenal au mwingine yoyote.
    "Hatutaki aondoke. Zaidi ya hapo, hakuna yeyote kutoka Arsenal ametoa aina yoyote ya ofa, si kwa Euro Milioni 27, au chochote," Perez aliliambia gazeti hilo la Hispania.
    New start: The striker could feature in Ancelotti's plans this season
    Mwanzo mpya: Mshambuliaji huyo anaweza kuwamo katika mipango ya Ancelotti msimu huu
    New targets: Liverpool's Luis Suarez (left) and Manchester United's Wayne Rooney (right) are wanted
    New targets: Liverpool's Luis Suarez (left) and Manchester United's Wayne Rooney (right) are wanted
    Walengwa wapya: Mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez (kushoto) na wa Manchester United, Wayne Rooney (kulia)  wanatakiwa Arsenal

    Inafikiriwa sasa Wenger amehamishia ndoana zake kwa mshambuliaji kinda wa miaka 20, Mfaransa Yaya Sanogo.
    The Gunners pia imetangaza ofa kwa mshambuliaji mtata wa Liverpool, Luis Suarez, na alipoulizwa kama amepanda dau la Pauni Milioni 40 kumnasa nyota huyo wa Uruguay, Wenger alisema kidogo.
    Wakati huo huo, kocha  David Moyes ameendelea kushikilia msimamo wake kwamba Wayne Rooney atabakia Manchester United- maana yake hilo ni pigo pia kwa Arsenal.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: RASMI HIGUAIN AMEOTA MBAWA ARSENAL...PEREZ ASEMA ANABAKI NA JUMATATU ATAKUTANA NAYE FARAGHA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top