• HABARI MPYA

    Sunday, April 19, 2015

    KOCHA AZAM ‘AZICHUKULIA POA’ SIMBA NA YANGA, ASEMA STAND UNITED NA MGAMBO NDIYO WANAMUUMIZA KICHWA

    George 'Best' Nsimbe kulia akiwa na Msaidizi wake, Dennis Kitambi

    REKODI YA GEORGE NSIMBE AZAM FC 

    Azam FC 1-0 JKT Ruvu (Ligi Kuu)
    Azam FC 1-0 Ndanda FC (Ligi Kuu)
    Azam FC 1-0 Coastal Union (Ligi Kuu)
    Azam FC 1-1 Mbeya City (Ligi Kuu)
    Azam FC 1-1 Mtibwa Sugar (Ligi Kuu)
    Azam FC 0-0 Mgambo JKT (Ligi Kuu)
    Azam FC 2-1 Kagera Sugar (Ligi Kuu)
    Na Princess Asia, DAR ES DALAAM
    KOCHA wa Mkuu wa Azam FC, George ‘Best’ Nsimbe amesema kwamba haumizwi kichwa na Simba na Yanga na kwamba mechi zinazomuumiza kichwa kati zilizobaki za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ni dhidi ya Stand United na Mgambo JKT.
    Tangu aanze kukaimu Ukocha Mkuu wa Azam FC miezi miwili iliyopita kufuatia kufukuzwa kwa aliyekuwa bosi wake, Mcameroon Joseph Marius Omog, Nsimbe ameshinda michezo minne na kutoka sare tatu.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana, kocha huyo wa Uganda amesema kwamba lengo lake ni kuhakikisha timu yake inashinda michezo yote iliyobaki ili kutetea ubingwa.
    Lakini Nsimbe amesema kwamba anaamini mchezo dhidi ya Stand United ni mgumu kuliko mechi dhidi ya Simba na Yanga. 
    “Simba na Yanga ni timu za kawaida, hivyo sina presha nazo, mechi ngumu kwangu ni za Stand na Mgambo, timu ambazo ziko chini zinahitaji kupata matokeo mazuri ili kujiweka nafasi nzuri”, alisema.
    Azam FC jana walizinduka kutoka kwenye sare tatu mfululizo, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Kwa ushindi huo, mabingwa hao watetezi wametimiza pointi 42, baada ya kucheza mechi 22, nyuma ya vinara, Yanga SC wenye pointi 46 za mechi 21.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOCHA AZAM ‘AZICHUKULIA POA’ SIMBA NA YANGA, ASEMA STAND UNITED NA MGAMBO NDIYO WANAMUUMIZA KICHWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top