• HABARI MPYA

    Monday, May 21, 2012

    ABIDAL ATOKA HOSPITALI


    Eric Abidal - Barcelona
    Eric Abidal - Barcelona
    BEKI wa Barcelona, Eric Abidal ameruhusiwa kutoka hospitali na ataendelea kujisikilizia hali yake nyumbani baada ya kufanyiwa upasuaji mapema mwaka huu.
    Beki huyo mwenye umri wa miaka 32, alifanyiwa upasuaji wa ini katika hospitali ya Barcaclinic, Aprili 10 ikiwa ni kiasi cha mwaka mmoja kuondolewa uvimbe.
    Abidal sasa amepwa ruhusa kurejea nyumbani, ambako ataendelea kupata ahueni akiwa karibu na familia yake.
    Hizi ni habari njema kwa The Blaugrana wakielekea kwenye Fainali ya Kombe la Mfalme, Copa del Rey dhidi ya Athletic Bilbao, Mei 25, mwaka huu ambayo itakuwa ni mechi ya mwisho kwa kocha Pep Guardiola kufanya kazi katika klabu hiyo.
    Abidal, aliyejiunga na Barca akitokea Olympique Lyonnais mwaka 2007, ameichezea timu hiyo mechi 38 kwenye mashindano yote msimu huu wa 2011-2012, kabla ya kufanyiwa upasuaji huo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ABIDAL ATOKA HOSPITALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top