Eric Abidal - Barcelona
BEKI wa Barcelona, Eric Abidal ameruhusiwa kutoka hospitali na
ataendelea kujisikilizia hali yake nyumbani baada ya kufanyiwa upasuaji mapema
mwaka huu.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 32, alifanyiwa upasuaji wa
ini katika hospitali ya Barcaclinic, Aprili 10 ikiwa ni kiasi cha mwaka mmoja
kuondolewa uvimbe.
Abidal sasa amepwa ruhusa kurejea nyumbani, ambako
ataendelea kupata ahueni akiwa karibu na familia yake.
Hizi ni habari njema kwa The Blaugrana wakielekea kwenye
Fainali ya Kombe la Mfalme, Copa del Rey dhidi ya Athletic Bilbao, Mei 25, mwaka
huu ambayo itakuwa ni mechi ya mwisho kwa kocha Pep Guardiola kufanya kazi
katika klabu hiyo.
Abidal, aliyejiunga
na Barca akitokea Olympique Lyonnais mwaka 2007, ameichezea timu hiyo mechi 38
kwenye mashindano yote msimu huu wa 2011-2012, kabla ya kufanyiwa upasuaji huo
0 comments:
Post a Comment