Anachotaka ni kujua moja tu, mustakabali wake inakuwaje?
MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Fernando Torres atakuwa na mazungumzo na klabu hiyo baada ya kukosoa jinsi anavyofanyiwa katika klabu hiyo.
Mspanyola huyo alisema ni moja ya mambo makubwa yaliyomsononesha kuanzishiwa becnhi katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich.
Torres alimuambia Mwandishi wa Kispanyola, Guillem Balague: "Nimekuwa na wakati mbaya sana katika msimu wangu huu.
"Nafikiri walikuwa wananichukulia katika namba ambayo sikuitarajia."
Mshambuliaji huyo wa Hispania, alisaini akitokea Liverpool kwa dau la pauni Milioni 50 Januari mwaka jana na amefunga mabao sita kwenye ligi katika ya 11 aliyofunga kwenye mashindano yote.
"Sijsikii vizuri. Ushindi kama huu dhidi ya Munich si kitu, lakini nataka waniambie itakuwaje katika mustakabali wangu.
"Sasa nafikiria kama soka ni mbaya, lakini nimepitia kipindi kigumu. Wananiharibia maisha. na sitaki kupitia huko tena."
Chelsea imepanga kuzungumza na mwakilishi wa Didier Drogba baadaye wiki hii kuangalia nafasi ya mchezaji huyo kubaki.
Klabu hiyo imekataa kumpa mkataba wa miaka miwili Drogba aliokuwa anautaka na iko tayari kumuongeza mwaka mmoja.
0 comments:
Post a Comment