TIMU ya soka ya taifa ya Gambia, The Scorpions inatarajiwa kuwasili leo usiku saa 3:20,
kikosini ikiwa na wachezaji 11 wanaocheza soka ya kulipwa nchi mbalimbali
Ulaya.
Wachezaji wa kulipwa wa Gambia watakaotua na ndege ya Kenya
Airways tayari kwa mechi ya Kundi C dhidi ya wenyeji Tanzania, Taifa Stars
Jumamosi kuwania tiketi ya kucheza Kombe la Dunia ni; Momodou Futty Danso wa Portland
Timbers ya Marekani, Lamin Basmen Samateh wa Hibernian F.C. ya Scotland, Pa
Saikou Kujabi wa NK Lokomotiva ya Croatia, Mustapha Kebba Jarju wa Mons ya
Ubelgiji, Yankuba Mal Ceesay wa Djurgardens IF ya Sweden,
Demba Savage wa HJK ya Finland, Alieu Darboe wa Le Mans ya
Ufaransa, Momodou Ceesay wa MSK Zilina ya Slovakia, Pa Modou Jagne wa FC St.
Gallen ya Uswisi, Tijan Jaiteh wa Randers FC ya Denmark na Omar Colley wa NK
Triglav ya Slevenia.
Wengine ambao wanacheaa nyumbani ni Musa Camara, Abdou
Jammeh, Ousman Koli, Saihou Gassama, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa
Yaffa, Sulayman Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe na Saloum Faal.
The Scorpions ilipaswa kubadili ndege Dakar, Senegal jana
usiku lakini kukawa na ucheleweshaji (delay), hivyo ikashindwa kuwahi Nairobi,
Kenya ambapo ingeunganisha kwa ndege ya alfajiri kuja Dar es Salaam.
Timu hiyo itafikia kwenye hoteli Sapphire iliyopo Mtaa wa
Lindi na Sikukuu eneo la Kariakoo, wakati waamuzi kutoka Zimbabwe ndiyo
watakaochezesha mechi hiyo.
Refa atakuwa Ruzive Ruzive na wasaidizi wake watakuwa ni
Salani Ncube na Edgar Rumeck, mwamuzi wa
akiba ni Norman Matemera na Kamisaa ni Fanie Wallace Mabuza kutoka Swaziland
wakati mtathmini wa waamuzi ni Ali Baligeya Waiswa.
Waamuzi hao watawasili nchini kesho (Juni 8 mwaka huu) saa
1.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways wakati Kamishna wa mechi hiyo atawasili
siku hiyo hiyo saa 12.50 jioni kwa ndege ya South African Airways na Mtathmini
wa waamuzi atatua pia Juni 8 mwaka huu saa 7.55 mchana kwa ndege ya Kenya
Airways.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager
inaendelea na mazoezi leo saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
chini ya Kocha Mkuu Kim Poulsen.
PROGRAMU YA MAZOEZI YA GAMBIA
IJUMAA JUNI 8
01.00 asubuhi Mazoezi- Uwanja wa Karume
10.00 jioni Mazoezi-
Uwanja wa Taifa
JUMAMOSI JUNI 9
04.00 asubuhi Mkutano
na Waandishi wa Habari- Ukumbi wa TFF
10.00 jioni Mazoezi-
Uwanja wa Taifa
0 comments:
Post a Comment