• HABARI MPYA

    Tuesday, June 12, 2012

    TENGA: YONDAN HAJA 'DOUBLE SIGN'


    Tenga leo

    RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Chillah Tenga amesema kwamba katika sakata la beki wa kimataifa wa Tanzania, Kelvin Patrick Yondan kudaiwa kusaini mara mbili, lazima kuna klabu moja imefanya uhuni, maana yake anamtetea beki huyo kwamba hajasaini mara mbili.
    Akijibu swali aliloulizwa kwenye Mkutano wake na Waandishi wa Habari mchana wa leo, ofisi za TFF, Ilala mjini Dar es Salaam, Tenga alisema kwamba kulingana na mfumo wa sasa wa usajili kupitia mtandao, shirikisho lake halihusiki kabisa na usajili na kwamba hilo ni suala la mchezaji na klabu.
    Tenga alisema anaamini klabu hizo zitamalizana zenyewe kuhusu mchezaji huyo na akasema suala la Yondan kudaiwa kutoroshwa kambini, Taifa Stars ili akasaini Yanga halina mantiki kwa sababu mchezaji huyo ni mtu mzima ana akili zake timamu, ila kinachoendelea kwa sasa ni kelele za kinazi.
    Wiki iliyopita, beki Yondan aliibuka anasaini Yanga, kabla ya klabu yake, Simba aliyoichezea tangu mwaka 2006 kudai bado ina mkataba naye na wapinzani wao hao wa jadi, wamefanya uhuni kuzungumza naye na kumsajili wakijua hajamaliza mkataba na klabu yake.
    Lakini Yondan mwenyewe alikana kusaini Simba na kusistiza amesaini Yanga tu, waliompa Sh. Milioni 30 kwa mkataba wa miaka miwili.   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TENGA: YONDAN HAJA 'DOUBLE SIGN' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top